Mhashamu
Baba Akofu Severin Niwemugizi wa jimbo Katoli la Rulenge Ngara akingia katika
Kanisa la Mt. Francisco parokia ya Biharamulo kutoa daraja la Upadre kwa
Shemasi Fortunatus Rweikiza.
|
Shemasi
Fortunatus Rweikiza muda mfupi kabla ya kupadirishwa katika Misa takatifu ya
Upadirisho katika Kanisa Katoliki la Mt. Francisco Parokia ya Biharamulo mkoani Kagera.
|
Askofu
Niwemugizi akimwekea mikono Padre Fortunatus kwa ajili ya Baraka.
|
Hapa
(Upadre Fortunatus Rweikiza ) ni baada ya kupadirishwa na kuvalishwa rasmi
Mavasi ya Upadre na Askofu Niwemugizi
ambaye ni Askofu wa Jimbo la Rulenge –Ngara .
|
Baada
ya Kupewa Daraja la Upadre (Upadre Fortunatus Rweikiza ) akaombewa ili kuitenda
kazi ya utume vizuri.
|
Askofu
Niwemugizi akimpaka mafuta ya Krisma aliyekuwa Shemasi Fortunatus Rweikiza.
|
Askofu
wa jimbo la katoliki la Rulenge-Ngara Mkoani Kagera, Mhashamu Severini Niwemugizi,Ijumaa ya ( Julai 12,2013) ametoa Daraja
la Upadre kwa aliyekuwa Shemasi Fortunatus Rweikiza.
Misa
takatifu ya Upadirisho kwa Padre Fortunatus imefanyika katika Kanisa Katoliki
la Mt. Francisco Parokia ya Biharamulo.
Aidha
katika hatua nyingine Askofu Niwemugizi ametoa wito kwa waumini wa Kanisa hilo
kujenga tabia ya kufunga ndoa na kuachana na dhana visingizio vya gharama kwa ajili ya harusi, na kuwataka wazazi kuhimiza
watoto wao kufunga ndoa na kukemea vikali visingizo vya mahari kwakuwa mambo
hayo hayana uhusiano na Kanisa .
Picha
Na: .ngarakwetu.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment