Old Bagamoyo Road yapatiwa jina la Rais Kibaki mjini Dar es Salaam. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, February 22, 2013

Old Bagamoyo Road yapatiwa jina la Rais Kibaki mjini Dar es Salaam.


Rais wa Kenya Mwai Kibaki  amefanya ziara nchini Tanzania ambayo ametumia kama njia ya kutoa mkono wa kwaheri wakati huu ambapo kenya inatarajia kufanya uchaguzi mkuu machi 4 mwaka huu.




Moja ya kumbukumbu kubwa aliyopata katika ziara yake ya kuwaaga watanzania waliopo jijini Dar Es Salaam ni kupewa jina lake katika moja ya barabara maarufu iliyokuwa ikijulikana kama Old Bagamoyo Road  na sasa inaitwa “MWAI KIBAKI ROAD".



Rais Kibaki akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete alizindua barabara hiyo Alhamis yenye jina  la barabara ya Mwai Kibaki.



Barabara hii kwa mujibu wa meya wa manispaa ya Kinondoni Rajab Mwenda ina historia ya kuwa imepita katika makazi ya Marais wote wa Tanzania tangu muasisi wa taifa la Tanzania  hayati baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere hadi Rais wa sasa Jakaya Kikwete.



Shughuli nyingine iliyofanyika katika ziara ya Rais Kibaki nchini Tanzania ni mazungumzo aliyoyafanya Rasi huyo wa Kenya na wazee wa mkoa wa Dar Es Salaam ambapo Rais Kibaki alisisitiza kuimarisha ushirikianao wa kibiashara baina  ya nchi hizi mbili ili kuchochea kasi ya maendeleo katika ukanda huu  wa Afrika mashariki.



Kenya na Tanzania zimekuwa katika uhusiano mzuri wa muda mrefu ambao umeimarishwa zaidi hivi  sasa katika mtengamano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki - EAC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad