![]() |
IGP .Said Mwema
|
Waliofikishwa
katika mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya hiyoAmoni Kahimba ni Boniphace John Kurwa(31),Gerard Tuti (33), David
Delina(36) wakulima wakazi wa Biharamulo na Bukoba na Zainabu Hamisi
Msabaha(26),fundi cherahani mkazi wa Biharamulo.
Mwendesha
mashitaka wa polisi Sajenti wa Polisi Paskael Nkenyenge Mahakama iliyofurika wasikilizaji kuwa katika muda
,siku wala tarehe isiyojulikana watuhumiwa hao walikamatwa kwa kosa la kula
njama za kufanya biashara haramu ya nyara za taifa kinyume na sheria ya kanuni ya
adhabu namba 384(16) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Alisema
watuhumiwa hao na wengine ambao hawajakamatwa Tuguro Zakayo,Nyarata
Mewama,Emanuel Kananjire(Mnyarwanda)ambao wanatafutwa wanakabiliwa na kosa hilo
.
Katika
kosa la pili Mwendesha mashitaha huyo aliliambia mahakama kuwa katika kosa la pili kuwa mnamo januari 4,2013
majira ya saa 5 usiku katika eneo la
Morotonga wilayani Serengeti alikamatwa na vipande 18 vya meno ya tembo vyenye
uzito wa kg 104 vyenye thamani ya T.Shilingi
Milioni 66,760,000= kinyume cha sheria.
Alisema
kosa hilo ni kinyume na sheria ya kanuni ya adhabu namba 86 kifungu cha 1,2 cha
sheria namba 5 ya mwaka 2009 pia kifungu cha 14(d)cha sheria za uhujumu uchumi
namba 60(ii) sura ya 200 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Kutokana
na kosa hilo la Uhujumu uchumi mshitakiwa hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa kosa hilo mpaka wapate kibali
cha mwendesha mashitaka wa
serikali(DPP).
Katika
kosa la kwanza washitakiwa wote walikana,na mwendesha mashitaka akaomba siku nyingine ya kutajwa kwa shitaka
hilo kwa kuwa upelelezi haujakamilika na
kuwa dhamana .
Hata
hivyo mwendesha mashitaka wa polisi Inspekta Msaidizi Abdallah Idd aliyekuwa
akishirikiana na Nkenyenge aliomba dhamana izingatie sheria namba 148 kifungu
cha (5)(e)kuwa wadhamini wawasilishe fedha taslimu zaidi ya Tanzania Shilingi
Milioni 10 au hati ya mali
isiyohamishika.
Hata
hivyo Hakimu Kahimba alitaka kujua sharti hilo ni kwa washitakiwa wote ama
mmoja ambapo mwendesha mashitaka
Nkenyenge alidai ni kwa mshitakiwa mmoja Kulwa,madai aliyoyakataa kwa madai
kuwa yanawahusu wote.
Mbali
na hilo aliwataka warekebishe mashitaka yao kwa kuwa hayaeleweki kwa kutoweka
muda na sehemu walikowakamatia inatia shaka ,na kuhoji wamejuaje wanastahili
kushitakiwa Mugumu na si kwingineko.
Akitoa
masharti ya dhamana Hakimu Kahimba alisema kila mshitakiwa anatakiwa ajidhamini
mwenyewe kwa dhamana ya Shilingi Milioni 2 ya maneno,pia mshitakiwa
atadhaminiwa na watu wawili wanaoaminika na kueleweka na wawe wakazi wa
Serengeti kwa dhamana ya Shilingi Milioni 10 za maneno.
Sharti
la tatu wadhamini ambao ni wakazi wa wilaya hiyo wanatakiwa kuweka fedha
taslimu milioni 34 mahakamani ama mali isiyohamishika yenye thamani ya zaidi ya
tsh,milioni.35.
Na
kuwa mali hiyo iwe na hati inayotambuliwa na imefanyiwa uthamini na mthamini anayetambulika na serikali na wala
si barua za watendaji ambazo amesema zimechangia watu wengi kukimbia kesi zao
na hawaeleweki.
Washitakiwa
,wadhamini na ndugu waliomba mahakama ilegeze masharti kwa madai kuwa wao ni wageni na hawawezi kuwapata
wadhamini wenye sifa hizo wilayani hapo.
Kabla
ya kutoa masharti ya dhamana alitoa angalizo kwa watu waliojitokeza kuwadhamini washitakiwa hao
wakati hawafahamiani na kuwa watanunua
kesi zisizowahusu.
Kesi
hiyo imeahirishwa hadi januari 28 mwaka huu itakapotajwa tena na watuhumiwa wote wamerudishwa mahabusu baada
ya kukosa wadhamini wenye sifa
zilizotajwa na Mahakama na kibali
kimetolewa watuhumiwa wengine watafutwe
ili waunganishwe na wenzao.
Kabla
ya kufikishwa Mahakamani hapo Tuti na Derina ambao walikuwa askari upepelezi Biharamulo na Kagera
walifukuzwa kazi januari 10,2013 baada
ya kupatikana na kosa kijeshi ili washitakiwe kiraia.
Washitakiwa hao walikamatwa Januari 6,mwaka
huu katika nyumba ya kulala wageni baada
ya Kurwa kuwataja na kubainika kuwa walikuwa askari kanzu kutoka Biharamulo na Kagera ambao ni D/c
Gerard Tuti mwenye namba za F5553 ambaye
ni mpelelezi katika ofisi ya kamanda wa makosa
ya jinai wilayani Bukoba .
Askari
mwingine ni D/c koplo David Delina mwenye namba E9172 kutoka ofisi ya upelelezi Biharamulo ambao walikuwa
na gari aina ya Toyota Ballon lenye namba za usajiri T403 BJK mali
ya mtuhumiwa David.
Mtuhumiwa
mwingine ni Boniphace John Kurwa(31)
ambaye ni raia mkazi wa Geita ambaye alikuwa na pikipiki yenye namba za usajili T784 CCC aina ya
Sunlog.
Ambaye
akiwa na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Nyarata akiwa na pikipiki yenye namba za usajili T 834 BPH
Toyo ambaye alitelekeza pikipiki na mizigo na kutokomea walikuwa wakitokea
kijiji cha Rwamchanga wakiwa na meno
hayo ambayo ni sawa na tembo watatu.
Januari
10 mwaka huu askari hao walifukuzwa kazi rasmi baada ya mashitaka ya kijeshi kukamilika na kubainika
kuwa walitenda kosa la jinai na hatimaye
januari 14 mwaka huu wakapandishwa katika mahakama ya
wilaya kujibu mashitaka yanayowakabili.
No comments:
Post a Comment