Pendelea kula Matunda na Mboga mboga ili upate faida zake katika mwili wako. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 18, 2012

Pendelea kula Matunda na Mboga mboga ili upate faida zake katika mwili wako.

Pendelea kula samaki upate faida zake katika kujenga mwili wako ,kwani
 -Huendesha mfumo wa kinga ya mwili
-Huzuia saratani
-Hutoa ahueni kwa wenye pumu
- Hupambana na dalili za awali za ugonjwa wa figo
-Huongeza nishati ya ubongo

-Huyeyusha damu, huifanya kuwa nyepesi
 - Huilinda mishipa ya damu isiharibike
-Huzuia damu kuganda
-Hushusha shinikizo la damu
-Hupunguza hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo na kiharusi
-Hutuoa ahueni kwa wenye ugonjwa wa kipandauso
-Husaidia kuzuia uvumbe mwilini.



Karoti

Karoti inaweza kuliwa mbichi, kupikwa na kuchanganywa na mbogamboga, kutengenezwa saladi na juisi. Faida zinazopatikana kutokana na utumiaji wa karoti ni kuongeza vitamini “A” ambayo inatokana na beta-carotene iliyomo ndani ya karoti na pia huongeza vitamini B, C, E na madini ya chuma mwilini. 


Karoti ina protini kidogo na haina mafuta ukilinganisha na mazao ya jamii ya kunde na yenye asili ya uwanga. Vile vile karoti ina nyuzi nyuzi (fiber) ambazo ni muhimu kwa kukinga kuta za utumbo na kulainisha choo. Karoti inasaidia kuongeza nuru ya macho, kukinga maradhi ya ngozi, magonjwa yenye asili ya kansa na kupunguza tindikali inayodhuru tumboni.


Inawezekana ukawa ni mvivu kuandaa juice si vibaya ukatumia matunda kama kifungua kinywa changanya matunda ya aina mbalimbali.


Juice ya matunda mbalimbali.


JUICE  YA KUTENGENEZA MWENYEWE NI NZURI ZAIDI KWA KUTUMIA HASA MATUNDA YA AINA MBALIMBALI, Pia kumbuka kwa kuifanya JUICE kama kifungua kinywa  ambapo husaidia kujenga afya iliyobora pia ni nzuri  kwa wale waliokuwa na nia ya kupunguza uzito na wanashauriwa kupendelea kunywa juice kuliko chai  au maziwa.


Kachumbari

Kachumbari ni moja kati ya vionjo katika chakula wengi hupenda kutumia kachumbari yenye mchanganyiko wa matunda ya aina mbalimbali kama nyanya, vitunguu maji, tango, parachichi, kabichi nk, kwa kuchanganya matunda haya unapata virutubisho vya asili katika mwili wako.

 

Vyakula vya aina mbalimbali

Unaweza kula kachumbari na vyakula vya aina mbalimbali kama pilau, ugali, ndizi, chipsi nk. lakini kwa waleambao wanapenda kupunguza uzito unaweza kufanya kachumbari kama chakula cha mchana kwa kuchanganya matunda ya aina mbalimbali.


Kwa kawaida, tunatakiwa kula matunda na mboga za majani kila siku, kiasi kisichopungua milo mitano.


 Lakini kwa bahati mbaya sana, siyo watu wote wenye fursa ya kupata na kula matunda kila siku. Hata wale wenye fursa hiyo, hawali inavyotakiwa.


Kitendo cha kutokula matunda hukosesha miili yetu virutubisho muhimu vya kujenga na kuimarisha kinga ya mwili, matokeo yake miili yetu inakuwa haina kinga ya kutosha.


 Mwili unapokuwa na kinga dhaifu, ni rahisi kushambuliwa na maradhi hatari, ikiwemo saratani, ambayo kinga yake kubwa iko kwenye ulaji wa matunda na mboga za majani.


Utashangaa kuona mtu anamaliza mwezi mzima hajala hata tunda moja. Msimu wa machungwa, kwa mfano, unaingia mpaka unaisha hajala hata chungwa moja. Ukija msimu wa maembe nao ni hivyo hivyo. 


Kuna mazoea ya kuona matunda siyo sehemu ya vyakula muhimu. Tabia hii ndiyo chanzo cha magonjwa mengi yanayotukabili hivi sasa.


Kwa upande mwingine, kuna makosa hufanyika wakati wa kula matunda. Kitaalamu inashauriwa kula matunda tumbo likiwa tupu, yaani kabla hujala kitu chochote tanguliza matunda kwanza na baada ya nusu saa au saa moja, ndiyo unashauriwa ule mlo wako kamili.


1 comment:

Post Bottom Ad