Siku chache
tuu baada ya mashetani wekundu Manchester United kumnasa rasmi aliekuwa Nahodha
wa Arsenal, Robin van Persie, Mchezaji Bora wa Ligi Kuu England kwa Msimu
uliopita na Msimu mpya wa Mwaka 2012/13 ukiwa unaanza Jumamosi Agosti 18,
Meneja wa Klabu Bingwa England Manchester City, Roberto Mancini, ameonyesha
kugwaya na usajili huo na kukiri usajili huo utaiboresha na kuiongezea nguvu
Manchester United.
Wiki
iliyopita Mancini alikiri Manchester United ina nafasi kubwa ya kuutwa Ubingwa
na leo akiongea na Wanahabari kuhusu Mechi yao ya Ufunguzi wa Ligi Kuu England
alisistiza msimamo wake huo hasa baada ya Man United kumnunua Nahodha wa
Arsenal, Robin van Persie.
Mancini
alitamka: “Ni wazi Manchester United wao wana nafasi kubwa ya kuutwaa Ubingwa.
Wao wamekuwa wakigombea Ubingwa kila Msimu kwa Miaka 20. Ingawa tumeshinda
Msimu uliopita lakini hiyo haibadili wao kuwa ndio Timu inayotegemewa kuwa
Bingwa! Na kwa kumchukua Van Persie, Mchezaji wa kiwango cha juu kabisa,
Straika Bora Msimu uliopita, na pamoja na Wayne Rooney watakuwa na Mastraika
hatari sana!”
Baadhi ya
watu wanasema Van Persie ingebidi aonyeshe upendo zaidi kwa Arsenal, baada ya
majeruhi yote ambayo aliyapata. Lakini kama nilivyosema mwanzoni, upendo wa
dhati siku hizi unatoka kwa mashabiki tu na hili jni jambo ambalo itabidi
likubaliwe.
Kwa
kuwaondoa wachezaji kama Ryan Giggs, Paul Scholes pale United na John Terry
pale Chelsea, hakuna wachezaji wanaoweza kudumu kwenye timu moja milele.
Arsenal sasa
tunajikuta kwenye wakati mgumu.
Klabu
imesajili washambuliaji kama Lukas Podolski kutoka Cologne, mshambuliaji wa
Ufaransa Olivier Giroud kutoka
Montpellier na kiungo wa Kispain Santi Cazorla kutoka Malaga, ambao
wanaweza kufanya vizuri kwenye EPL.
Van Persie
alijiunga na Gunners mwezi May 2004, muda mchache baada ya klabu yangu ya
zamani kumaliza msimu bila kufungwa katika ligi kuu ya England.
Aidha kila mwaka baada ya mwaka, wachezaji wakubwa
waliondoka ambapo Jens Lehman, Ashley Cole, Sol Campbell, Robert Pires, Thierry
Henry na Patrick Vieira wote wakaondoka.
Na tangu
awasili kutoka Feyenoord, Van Persie aliweza kushinda kombe moja tu - FA Cup,
miaka saba iliyopita.
RATIBA
MECHI ZA UFUNGUZI:
Jumamosi
Agosti 18
[Saa
11 Jioni]
Arsenal
v Sunderland
Fulham
v Norwich City
Newcastle
United v Tottenham Hotspur
Queens
Park Rangers v Swansea City
Reading
v Stoke City
West
Bromwich Albion v Liverpool
West
Ham United v Aston Villa
Jumapili
Agosti 19
[Saa
9 na Nusu Mchana]
Wigan
Athletic v Chelsea
[Saa
12 Jioni]
Manchester
City v Southampton
Jumatatu,
Agosti 20
[Saa
4 Usiku]
Everton
v Manchester United
No comments:
Post a Comment