Baada ya polisi kuua wachimba migodi 34, wake wa wachimbaji waandamana. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 18, 2012

Baada ya polisi kuua wachimba migodi 34, wake wa wachimbaji waandamana.

Wake za wachimba madini wakiandamna jananchini Afrika kusini kutokana na Polisi wa nchi hiyo kuua wachimbaji 34 na kuwajeruhi kadhaa baada ya wachimbaji hao kufanya mgomo na kuandamana kudai maslahi yao.


Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameelezea kusikitishwa na tukio hilo la mauaji  ya wachimba madini 36 wa nchi hiyo na kutoa wito wa kufanyika uchunguzi wa haraka kuhusiana na tukio hilo.


Aidha Rais Zuma ametoa amri ya kuundwa tume maalumu ya kuchunguza tukio hilo na waliohusika kuchukuliwa hatu.


Polisi wakiweka kambi mbele ya waandamanaji nje kidogo ya mji wa Rustenburg, km 62 kaskazini magharibi mwa mji wa Johannesburg, Ambapo juzi August 16 waliwapiga risasi wachimba madini 34 wakati maalfu ya wachimba madini hao walipo goma na kuandamana kunadai maslahi zaidi.

 

Ripoti zinasema kuwa, kikosi cha kuzuia fujo cha Afrika Kusini kiliwafyatulia risasi wafanyakazi wa mgodi wa platinum na kuua watu wasiopungua 36.


Mauaji hayo yametokeakwenye eneo ambapo wachimbaji walipigwa hapo juzi kwenye mgodi wa Lomin karibu na mji wa Rustenburg Afrika kusini.



Vyombo vya usalama vya Afrika Kusini vinadai kuwa wafanyakazi wa mgodi huo walikuwa wamejidhaatiti kwa silaha tayari kushambulia jeshi la polisi.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad