Mtanzania ashindwa kuwika kwenye michuano ya Olimpiki 2012 - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, August 07, 2012

Mtanzania ashindwa kuwika kwenye michuano ya Olimpiki 2012

Mshiriki wa michuano ya Olimpiki kutoka Tanzania, Zakia Mrisho, leo ameshindwa kufurukuta baada ya kuambulia nafasi ya 31 kati ya washiriki 34 waliokimbia mbio za mita 5000 kwa wanawake. Zakia amekimbia umbali huo kwa dakika 15 na sekunde 39.



Aidha Fainali ya Wanawake ya Mashindano ya OLIMPIKI LONDON 2012 itakuwa ni kati ya Mabingwa wa Dunia Japan  na Mabingwa watetezi wa Olimpiki Marekani ama  USA  baada ya Timu hizo kushinda Mechi zao za Nusu Fainali hapo jana kwa Japan kuichapa Ufaransa  2-1 Uwanjani Wembley na USA katika  Uwanjani Old Trafford, kuendeshwa mchakamchaka na Canada wa Dakika 120 kufuatia sare ya bao 3-3 katika Dakika 90 na kupata bao la 4 na la ushindi katika Dakika ya 122 na Sekunde 28.


USA  ambao wamecheza Fainali zote za Olimpiki tangu kwa Soka kwa Wanawake iingie kwenye Michezo ya Olimpiki Mwaka 1996 hivyo kufanya  Fainali ya Japan  maarufu kama Nadeshiko maana yake ‘UA ZURI la PINKI’  na USA  kuzikutanisha Timu zilizokutana Fainali ya Kombe la Dunia Mwaka jana na Japan kuibwaga USA kwa Mikwaju ya Penati.


Fainali hii ni ya  kugombea Medali ya Dhahabu, itachezwa Alhamisi Agosti 9 Uwanjani Wembley na itatanguliwa na Mechi ya kuwania Ushindi wa Tatu kati ya France na Canada na Mshindi wake atapata Medali ya Shaba.


Leo (Jumanne) Usiku ni Nusu Fainali za Wanaume kati ya Mexico na Japan na itafuatia ile ya Korea Kusini na Brazil.


     Olimpiki 2012: Orodha ya medali.
Nafasi Nchi Medali za dhahabu   Medali za fedha   Medali za shaba  Jumla
1Uchina Uchina32191465
2MarekaniMarekani29151963
3UingerezaUingereza19121243
4Korea KusiniKorea Kusini115622
5FranceFrance891027
6Urusi Urusi 7171842
7ItaliaItalia76417





         

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad