WAZIRI WA FEDHA DK. WILLIAM MGIMWA AWASILISHA BAJETI YA MWAKA 2012/2013 BUNGENI ' - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, June 14, 2012

WAZIRI WA FEDHA DK. WILLIAM MGIMWA AWASILISHA BAJETI YA MWAKA 2012/2013 BUNGENI '

Waziri wa Fedha, Dkt. William Mgimwa akisoma bajeti ya Serikali  ya 2012/13, Bungeni Mjini Dodoma Juni 14, 2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Waziri wa fedha na uchumi Dk William Mgimwa leo amewasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ambayo nin sh Trilioni 15 tofauti na ile ya mwaka unaomalizika ya Sh Trilioni 13.5,katika mwaka ujao wa fedha ambao huanza Mwezi July ya kila mwaka.


Bajeti hiyo ina vipaumbele 7 ambavyo ni Miundombinu, kilimo, viwanda, rasilimali watu, huduma za jamii, utalii, pamoja na biashara ya ndani na nje na huduma za fedha.

 

Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa  akionyesha mkoba wenye Bajeti ya Serikali ya  2012/13 Bungeni Mjini Dodoma Juni 14, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

Bajeti hiyo imeelezwa kuwa itakuwa mwiba kwa mtanzania ambapo baadhi ya bei za bidhaa (vinywaji na vileo )zimeongezwa kodi hali ambayo ilisababisha migumo miongoni mwa wabunge na baadaye kutoa maoni yao.

Aidha waziri huyo ametangaza kuanza kwa mafunzo yay a lazima ya JKT kwa mwaka huu ambapo jumla ya vijana 5000 wataanza mafunzo hayo pamoja na kutangaza kuajiri zaidi ya wataumishi elfu 70 katika sekta mbalimbali.

 

Mabalozi wa Nchi mbalimbali  waliohudhuria Bungeni kusikiliza Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2012/13 iliyosomwa na Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa, Bungeni Mjini Dodoma Juni 14,2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

Bajeti imelenga kuviwezesha viwanda vya ndani kuhimili soko la ushindani kwa bidhaa zake dhidi ya bidhaa zinazoagizwa kutoka nje.


Hali kadharika Bajeti hiyo imetoa pendekezo la kulinda kazi za wasanii kwa kusajili kazi hizo ili kuwaingizia faida ya kipato kitakacho wawezesha kunufaika na kazi zao.


Jeh! bajeti hii inayosomwa leo inakugusa kiasi gani Mtanzania mwenzangu?



WAKATI HUO HUO  BAJETI YA SMZ YAWASILISHWA LEO MJINI ZANIZBAR BAJETI YA SMZ YAWASILISHWA LEO MJINI ZANIZBAR .


Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetangaza Bajeti yake kwa mwaka 2012/13 ambayo pamoja na mambo mengine, imeongeza kodi katika maeneo manane ikiwamo mafuta, ada ya bandari na ushuru wa stempu huku ikiwa na maeneo sita ya kipaumbele.

 

 

Maeneo hayo ya vipaumbele ni afya, ajira kwa vijana, ustawi wa wazee, elimu, kuimarisha uchumi na kuhifadhi mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.





Waziri wa Nchi Afisi ya Rais anaeshughulikia Fedha na Uchumi na
Mipango ya Maendeleo Zanzibar,Omar Yussuf Mzee akionesha mkoba wenye nyaraka za  Bajeti ya
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 leo Nje
ya Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi(Picha na Yussuf Simai,MAELEZO
Zanzibar)

 

SMZ katika bajeti yake hiyo, imepanga kutumia Sh307.8 bilioni kwa kazi za kawaida na Sh341.1bilioni kwa ajili ya shughuli za maendeleo huku makusanyo yakitarajiwa kuwa 648.9 bilioni.


Akiwasilisha Bajeti hiyo jana kwenye Baraza la Wawakilishi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo), Omar Yussuf Mzee alisema kwa kuzingatia dhamira ya Serikali katika kukuza mpango wa maendeleo, imependekeza marekebisho ya viwango vya tozo ya kodi.



Waziri wa Nchi Afisi ya Rais anaeshughulikia Fedha na Uchumi na
Mipango ya Maendeleo Zanzibar,Omar Yussuf Mzee akisoma bajeti ya SMZ
  leokatika Baraza la Wawakilishi.(Picha na Yussuf Simai,MAELEZO
Zanzibar)

 

Mzee alitaja mabadiliko hayo kwamba yamegusa  Sheria ya Ushuru wa Stempu namba 6 ya mwaka 1996, Sheria ya Kodi za Hoteli namba 1 ya mwaka 1995, Sheria ya Ada za Bandari namba 2 ya mwaka 1999 na Sheria ya Ushuru wa Petroli namba 7 ya mwaka 2001.

 

Sheria nyingine ni ile ya Usimamizi na Utaratibu wa kodi namba 7 ya mwaka 2009, Sheria ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) namba 4 ya mwaka 1998, Sheria ya Bodi ya Mapato Zanzibar namba 7 ya mwaka 1996 na Sheria ya Mafunzo ya Amali namba 8, ya mwaka 2006.

 




 

.

 


 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad