Mratibu wa mradi katika shirika la TCRS wilayani Ngara Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya maafisa watendaji wa vijiji ni kikwazo cha maendeleo katika vijiji wanavyoviongoza - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 17, 2012

Mratibu wa mradi katika shirika la TCRS wilayani Ngara Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya maafisa watendaji wa vijiji ni kikwazo cha maendeleo katika vijiji wanavyoviongoza

Mto Ruvubu ambao huanzia nchini Burundi na kupita Ngara ,kisha kukutana na mto Kagera na kutengeneza maporomoko ya Rusumo-Tanzania.

Mratibu wa mradi katika shirika la TCRS wilayani Ngara Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya maafisa watendaji wa vijiji ni kikwazo cha maendeleo katika vijiji wanavyoviongoza.

Bw Nkya amesema watendaji hao wanafanya kazi kwa maslahi binafsi badala ya maslahi ya jamii wanayoitumikia  na hivyo kushindwa kuwa chachu ya uongozi bora.

Hali ya ukungu ambao huja wakati wa masika ukiambatana na Mvua wilayani Ngara mkoani Kagera.

Amesema baadhi ya watendaji wamekuwa wakijaribu kukwamisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati za vijiji kwa kuhofia kuwa endapo kamati husika zitapata uelewa zitawabana na kushindwe kufanya ubadhirifu.

 

Aidha Bw Nkya amewataka watendaji kutambua kuwa wamepewa nyadhifa hizo ili kuwatumikia wananchi badala ya kuendekeza maslahi yao binafsi.

 

''Ngara is one of the seven Districts in Kagera region. It is in the extreme north west of Tanzania . It borders Rwanda in the North; Burundi in the Southwest; Biharamulo in the East, Karagwe in the North East and Kibondo in the South. The distance from Ngara to Dar es Salaam is 1,600 Km and to the regional headquarters, Bukoba is 350 kms. The tarmac road connects Ngara with Kigali in Rwanda , Bujumbura in Burundi and to the dry port of Isaka . The area of Ngara is km 2 3,744 and it is divided into four divisions, 17 wards and 72 villages. It is further subdivided into 359 sub villages ( vitongoji). 

Katika hatua nyingine,Afisa mtendaji wa kijiji cha Kazingati kata ya Keza wilayani Ngara Bw Philip Kasigwa amekanusha madai ya wananchi wa kijiji hicho kuwa anauza  ardhi ya wafugaji wa kijiji hicho na kwamba  madai ya wananchi hao ni majungu dhidi yake na kwamba hakuna ardhi iliyouzwa .


Hivi karibuni wakazi wa kijiji cha kazingati walimuomba mwenyekiti wa kijiji hicho kuitisha mkutano ili kupiga kura ya kutokuwa na imani na mtendaji huyo kwa madai kuwa anajihusisha uuzaji wa ardhi ya wafugaji .

 

Makundi ya ng'ombe ambayo huonekana katika ardhi na mapori mbalimbali wilayani Ngara.

Aidha mwenyekiti wa baraza la vijana la Chadema wilayani Ngara Bw Nestory Mashishanga amesema wananchi wanapaswa kushirikishwa katika mambo muhimu kuhusu kijiji chao
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad