MKOA WA KAGERA WAPATA USAFIRI WA PIKIPIKI KWA AJILI YA KUKUSANYIA TAKWIMU ZA KILIMO VIJIJINI. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, June 29, 2012

MKOA WA KAGERA WAPATA USAFIRI WA PIKIPIKI KWA AJILI YA KUKUSANYIA TAKWIMU ZA KILIMO VIJIJINI.


Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh. Kanali mstaafu Fabiani Massawe akikabidhi pikipiki kwa wawakilishi wawakurugenzi wa halmashauri za wilaya na manispaa.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera amekabidhi pikipiki nane kwa wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na manispaa ya Bukoba kwa ajili ya kukusanya taarifa na takwimu mbalimbali za kilimo kutoka vijijini katika mkoa wa Kagera.

Pikipiki hizo zimetolewa na serikali ya Tanzania kupitia wizara ya kilimo, chakula na ushirika ikishirikiana na shirika la Kimataifa la uhusiano la nchini Japan (Japan International Cooperation Agency, (JICA) ambalo limewakilishwa na Bi. Akasaka Kyoko wakati wa kukabidhi pikipiki hizo nane.

 


Pikipiki zilizotolewa na JICA

 Mhe. Massawe pia amewasistiza sana wakurugenzi wa halmashauri na manispaa kutunza pikipiki hizo na kuzifanyia kazi iliyokusudiwa na si vinginevyo. Aidha aliwaomba maafisa kilimo watakaozitumia pikipiki hizo kukusanya takwimu za kweli ili kuondokana na tatizo la takwimu zisizo sahihi. 

Pamoja na pikipiki hizo, JICA pia waliendesha mafunzo ya ukusanyaji takwimu na kugawa kompyuta moja na “flash” moja kwa kila halmashauri ya wilaya na manispaa kwa ajili ya kukusanya na kutunza takwimu za kilimo vijijini.

Mkuu wa Mkoa aliwashukuru JICA kwa kujitolea kuleta maendeleo Tanzania na hasa katika mkoa wa Kagera. Ambapo pia amewahakikishia JICA kuwa serikali itaendelea kuhamasisha wananchi kuondokana na kilimo cha kuchumia tumbo na kujikimu na kuhamia katika kilimo cha biashara zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad