Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wamekuwa wakiwaonea wananchi kwa kuwa hawajui namna ya kuwawajibisha viongozi - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, June 29, 2012

Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wamekuwa wakiwaonea wananchi kwa kuwa hawajui namna ya kuwawajibisha viongozi



Mratibu wa mradi katika shirika la TCRS wilayani Ngara mkoani Kagera Bw Eveready Nkya amesema baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wamekuwa wakiwaonea wananchi kwa kuwa hawajui namna ya kuwawajibisha viongozi hao wanaposhindwa kuwajibika ipasavyo.


Bw Nkya amesema hayo leo katika kipindi cha mada kilichotamgazwa na radio Kwizera kuhusu tija ya maadhimisho ya siku ya serikali za mitaa nchini.


Amesema baadhi ya wenyeviti wa vitongoji, vijji na watendaji wa vijiji na kata wamekuwa wakitumia udhaifu wa wananchi kutotambua haki zao na kuwaendesha jinsi wanavyotaka wao jambo ambalo ni kinyume na taratibu.


Bw Nkya amesema juhudi za ziada zinahitajika kwa mashirika mbalimbali kusaidiana na serikali katika kutoa elimu kwa viongozi wa serikali za mitaa ili kuboresha utendaji kazi na kuchochea maendeleo ya jamii kwa ujumla.




Kwa upande wake Afisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya ngara Bw Martin Kanyambo amesema Elimu duni ya uraia kwa viongozi wa serikali za mitaa imetajwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazokwamisha ufanisi katika uwajibikaji wa viongozi husika kwa wananchi hali inayokwamisha pia maendeleo katika maeneo wanayoyaongoza.


Aidha Bw Kanyambo amesema kuwa serikali inajitahidi kutoa elimu ya uraia kwa viongozi wa serikali za mitaa kuanzia ngazi za vitongoji pamoja na wananchi kwa ujumla ili kurahisisha maendeleo katika jamii.

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad