WADOKOZI WABAMBWA NA POLISI JAMII KATIKA MJI MDOGO WA RULENGE-NGARA MKOANI KAGERA WAKIIBA BIDHAA DUKANI. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 02, 2012

WADOKOZI WABAMBWA NA POLISI JAMII KATIKA MJI MDOGO WA RULENGE-NGARA MKOANI KAGERA WAKIIBA BIDHAA DUKANI.

Na :Shaaban Ndyamukama - Ngara ,Kagera.

Vijana wawili wakazi wa mji mdogo wa Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera wanashikiliwa na jeshi la polisi wilayani humo baada ya kudokoa bidhaa mbalimbali katika maduka ya wajasiliamali jumatatu wiki hii


Vijana hao ni Shabani Jacobo ( 37) na Godfrey Turbo (27 ) waliingia katika duka la mfanyabiashara Ismail Mulengera  wa mji  wa Rulenge kutafuta bidhaa kuwaletea wateja wake na walipofika ndani ya stoo walianza kukwepesha baadhi ya mali na katika kuficha ndipo wakabambwa na mwenye duka 


Wananchi waliowakamata  waliwakuta na katoni mbili za sabuni na makasha mawili ya amila aina ya pasha na kuanza kupata kipondo wameokolewa na polisi jamii kituo cha rulenge na kufungwa kamba kwa ajili ya kuokoa maisha yao na kufunguliwa mashtaka.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad