MOJA YA MADUKA KATIKA SOKO KUU LA KIGOMA MJINI LIMEWAKA MOTO HUKU JESHI LA POLISI MKOANI HUMO LIKIFANIKIWA KUDHIBITI MOTO KATIKA YA SOKO KUU MKOANI HUMO. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, March 30, 2012

MOJA YA MADUKA KATIKA SOKO KUU LA KIGOMA MJINI LIMEWAKA MOTO HUKU JESHI LA POLISI MKOANI HUMO LIKIFANIKIWA KUDHIBITI MOTO KATIKA YA SOKO KUU MKOANI HUMO.

Eneo la tukio la moto soko la Kigoma kibanda namba 16A ambapo Kikosi cha zima moto wakiwa wamefaulu kudhibiti moto huo katika ajali ya moto  katika Soko hilo.
Wananchi wakishanga juhudi za polisi na zimamoto wakikabiliana na moto huo huku Freezer linalodhaniwa ndio chanzo cha moto huo hapa chini.
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa  kuzuia na kuokoa  mali  na kudhiti moto kwa kushirikiana na askari zima Moto wa kikosi cha zimamoto Halmashauri ya Kigoma Ujiji na Kikosi cha zimamoto viwanja vya Ndege na baadhi ya vitu vimeokolewa na vingine kuungua bado thamani yake haijajulikana.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Kihenya Kihenya  amemtaja mmiliki wa duka hilo kuwa ni Faustine  Samweli 39, Mfanyabiashara wa Lumumba  Road chumba NO.16 kiliungua moto.

Kaimu Kamanda  amesema kuwa  Chanzo cha moto huo ni Freezer iliyokuwa imeachwa ikiwaka usiku mzima bila kuzimwa hivyo kusababisha chanzo cha moto huo.

Kamanda huyo amesema kuwa Thamani halisi ya mali iliyoteketea bado haijajulikana  na uchunguzi zaidi wa tukio hilo bado unaendelea.

Hata hivyo kamanda kihenya amewataka wafanya biashara wa eneo hilo kuhakikisha usalama wa mali zao kabla na baada ya kufanya shughuli zao kuwa waangalifu wakati wa ufungaji wa maduka yao ili kuzuia tukio la aina hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Issa Machibya akitazama juhudi za askari Polisi na Zima Moto wa kuokoa mali na Kufanikiwa kudhibiti moto huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad