Waziri Kalemani awasha Umeme Kasharazi na Kukagua Maendeleo ya Mradi Rusumo, Ngara. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Sunday, June 10, 2018

demo-image

Waziri Kalemani awasha Umeme Kasharazi na Kukagua Maendeleo ya Mradi Rusumo, Ngara.

.com/simgad/
34847119_1888982887808279_2132211178087120896_n
Hapa ni ndani ya eneo la Mradi wa umeme Rusumo  ambapo Mawaziri wote wa pande mbili Waziri wa Miundombinu Rwanda Clever Gatete, Waziri wa Nishati Rwanda Kamayirese Germaine  na Waziri wa Nishati wa Tanzania Dkt.Medard Kalemani walipata maelezo kuhusu maendeleo ya mradi huo wa umeme wa maporomoko ya maji.
 34847770_1888982967808271_5912796298611785728_n
 34875245_1888983091141592_1509298688030146560_n
35121257_1888983047808263_8364914503673970688_n

Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani akibonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya kuanza kupatikana kwa huduma ya umeme katika Kitongoji cha Gwingwe ,Kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera. Na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Michael Mtenjele.


Katika ziara hiyo pia, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani alizindua na kuwasha umeme wa TANESCO katika Kijiji cha Kasharazi, Kitongoji cha Gwingwe wilayani Ngara Mkoani Kagera.

Wakati wa uzinduzi huo Kijijini hapo, Waziri Kalemani amesema ili Tanzania ipate maendeleo ni muhimu vijiji vyote vikapata umeme wa uhakika.

Amesema ni vyema sasa wakandarasi waliokabidhiwa jukumu la kusambaza umeme vijijini wafanye jitihada hizo haraka ili vijiji vyote vipate umeme kwa wakati.

Hata hivyo Waziri Kalemani amewataka wananchi kuitunza vyema miundo mbinu hiyo kwakua ina manufaa kwao na kizazi kijacho.

Waziri wa Nishati ilifungua matumizi ya umeme wa Gridi ya Taifa wilayani Ngara,mkoani Kagera Aprili 8 ,2018 huu hivyo kuwezesha Wilaya hiyo kuachana na matumizi ya umeme wa mafuta.

Kazi iliyobaki ni kuunganisha upande mwingine wa nchi ambao unaanzia Mbeya kupitia Sumbawanga, Kigoma, Mpanda, Nyakanazi hadi Geita na Bulyanhulu  inatarajiwa kukamilika ifikapo 2020/2021.34906653_1888983097808258_4681758555890515968_n
Pia Waziri kalemani alitembelea na Kukagua Maendeleo ya Mradi wa Umeme Rusumo.
 35082758_1888983117808256_7591294256900210688_n
 34877823_1888982987808269_374847621560270848_n

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *