Waziri Kalemani awasha Umeme Kasharazi na Kukagua Maendeleo ya Mradi Rusumo, Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 10, 2018

Waziri Kalemani awasha Umeme Kasharazi na Kukagua Maendeleo ya Mradi Rusumo, Ngara.

Hapa ni ndani ya eneo la Mradi wa umeme Rusumo  ambapo Mawaziri wote wa pande mbili Waziri wa Miundombinu Rwanda Clever Gatete, Waziri wa Nishati Rwanda Kamayirese Germaine  na Waziri wa Nishati wa Tanzania Dkt.Medard Kalemani walipata maelezo kuhusu maendeleo ya mradi huo wa umeme wa maporomoko ya maji.
 
 

Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani akibonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya kuanza kupatikana kwa huduma ya umeme katika Kitongoji cha Gwingwe ,Kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera. Na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Michael Mtenjele.


Katika ziara hiyo pia, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani alizindua na kuwasha umeme wa TANESCO katika Kijiji cha Kasharazi, Kitongoji cha Gwingwe wilayani Ngara Mkoani Kagera.

Wakati wa uzinduzi huo Kijijini hapo, Waziri Kalemani amesema ili Tanzania ipate maendeleo ni muhimu vijiji vyote vikapata umeme wa uhakika.

Amesema ni vyema sasa wakandarasi waliokabidhiwa jukumu la kusambaza umeme vijijini wafanye jitihada hizo haraka ili vijiji vyote vipate umeme kwa wakati.

Hata hivyo Waziri Kalemani amewataka wananchi kuitunza vyema miundo mbinu hiyo kwakua ina manufaa kwao na kizazi kijacho.

Waziri wa Nishati ilifungua matumizi ya umeme wa Gridi ya Taifa wilayani Ngara,mkoani Kagera Aprili 8 ,2018 huu hivyo kuwezesha Wilaya hiyo kuachana na matumizi ya umeme wa mafuta.

Kazi iliyobaki ni kuunganisha upande mwingine wa nchi ambao unaanzia Mbeya kupitia Sumbawanga, Kigoma, Mpanda, Nyakanazi hadi Geita na Bulyanhulu  inatarajiwa kukamilika ifikapo 2020/2021.
Pia Waziri kalemani alitembelea na Kukagua Maendeleo ya Mradi wa Umeme Rusumo.
 
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad