![]() |
Mashindano
hayo yamehudhuriwa na Naibu Waziri waNchi, OR – TAMISEMI, Joseph Kakunda, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Juliana Shonza, Mkuu wa
Mkoa wa Mwanza, John Mongella pamoja
na viongozi mbalimbali wa Serikali, Wadhamini wa Mashindano hayo, Wadau wa
michezo na baadhi ya wananchi wa mkoa wa Mwanza.
|
Mkurugenzi
Nyanza Bottling Company Ltd Christopher
Gachuma akisalimaina na Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Aidha,
amewataka wanafunzi wanaoshiriki mashindano hayo watumie ushiriki wao kwa
kuuthibitishia umma dhamira waliyonayo ya kuonesha kuwa, zipo fursa nyingi za
ajira endapo vipaji vya michezo na sanaa vitatumika kikamilifu.
Amesema
uhalali wa michezo na mashindano shuleni unatajwa katika Ilani ya Uchaguzi ya
CCM ya 2015-2020, Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995, Sera ya
Elimu ya mwaka 2014 ambazo kwa pamoja zinaelekeza kutambua na kuendeleza vipaji
vya wanafunzi shuleni kufikia malengo ya maendeleo endelevu.
|
Kaulimbiu ya
Mwaka huu 2018 inasema MICHEZO ,SANAA NA TAALUMA NI MSINGI WA MAENDELEO YA
TAIFA .
Katika hatua
nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa amewaagiza Maafisa Elimu wa Mikoa na
Wilaya wahakikishe maeneo ya michezo na burudani yanapimwa na yasiingiliwe, pia
vitengo vya michezo kwenye ofisi za Halmashauri na Mikoa vitengewe fedha za
kuendeshea michezo.
|
Wanafunzi wa
UMISETA wakiimba wimbo wa alaiki uwanja
wa CCM Kirumba Mwanza.
Waziri Mkuu
Majaliwa amesema Vipaji vya Michezo na Sanaa vitaitangaza nchi kimataifa na kuongeza
fursa ya ajira kwa Watanzania.
Amesema kauli mbiu ya michezo ya UMISSETA na
UMITASHUMTA ya mwaka huu ni “michezo, sanaa na taaluma ni msingi wa
maendeleo ya mwanafunzi katika Taifa letu”.
|
Mashindano
hayo yanafanyika kwa mara ya 3 mfululizo
katika Jijini Mwanza pamoja na kampuni ya COCA COLA kwa kudhamini michezo
ya mpira wa miguu na kikapu kwa Shule za Sekondari na kampuni ya AZAM kwa kujitolea
kuonesha michezo hiyo kwa mwaka huu.
|
No comments:
Post a Comment