Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2017/2018 imefikia Tamati yake
Jumatatu May 28, 2018 kwa michezo 15 kuchezwa katika viwanja mbalimbali ambapo,
Yanga SC wakiwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam wamekutana na kipigo cha magoli
3-1 kutoka Azam FC.
Magoli ya Azam FC katika mchezo huo yakifungwa na Yahaya Zayd dakika ya 4,
Shaban Iddi dakika ya 60 na Salum Abubakar dakika ya 68 wakati goli pekee la
Yanga SC lilifungwa na Abdallah Kheri wa Azam FC aliyejifunga.
|
Kipigo hicho sasa kinaifanya Yanga SC kumaliza Ligi wakiwa nafasi ya tatu
nyuma ya Azam FC waliyopo nafasi ya pili, wakati Timu ya Majimaji FC ya Songea
baada ya kutoa sare ya 1-1 na Mabingwa wapya wa Ligi hiyo Simba SC wanaungana
na Njombe Mji FC kushuka daraja.
|
Simba SC, zamani ikijulikana kama Sunderland msimu huu imetwaa taji la 19
baada ya awali kubeba katika miaka ya 1965, 1966 (kama Sunderland), 1972, 1973,
1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1993, 1994, 1995, 2001, 2002, 2004, 2007, 2009–10
na 2011–2012.
Lakini mahasimu wao, Yanga SC wanabaki kuwa Mabingwa mara nyingi wa Ligi Kuu, baada ya kubeba taji mara 27 katika miaka ya 1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1987, 1991, 1996, 1997, 2000, 2005, 2006, 2007–2008, 2008–2009, 2010–2011, 2012–2013, 2014–2015, 2015–2016 na 2016–2017. Timu nyingine zilizowahi kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ni Cosmopolitans 1967, Pan African 1982, Azam FC 2013-2014 zote za Dar es Salaam, Mseto SC 1975, Mtibwa Sugar 1999 na 2000 zote za Morogoro, Tukuyu Stars ya Mbeya 1986 na Coastal Union ya Tanga 1988. |
Very nice poost
ReplyDelete