Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Mwalimu Kasuku Bilago alifikwa na umauti
wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jumamosi May 26,
2018,jijini Dar es Salaam.
Mwalimu Bilago
alizaliwa Tarehe 2/2/1964 na amefariki akiwa Mbunge wa kuchaguliwa wa Jimbo la
Buyungu mkoani Kigoma ambapo alichaguliwa mwaka 2015.
|
Naibu Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson akifungua kikao cha Bunge kwa
kusoma dua, alitoa Bungeni hapo Taarifa ya Spika kuhusiana na msiba huo mzito
uliolifika Bunge, na baade kutangaza kuahirisha Bunge hadi leo Jumanne May 29
saa tatu asubuhi, ili kupisha Maombolezo huku mipango ya kuuleta mwili katika
viwanja vya Bunge kwa heshima za mwisho ikifanyika.
Mwili wa Marehemu Bilago unataraji kuletwa Bungeni leo May 29, 2018 kwa
heshima za mwisho na baade kusafirishwa hadi Kijiji cha Kasuga Wilaya ya
Kakonko Mkoani Kigoma ambako utahifadhiwa May 31, 2018.
|
Baada ya
kuagwa Karimjee, mwili wa Marehemu Bilago utasafirishwa kwenda Dodoma ambapo Leo
Jumanne May 29, utaagwa na wabunge wote, bungeni Jijini Dodoma kabla ya
kusafirishwa kwenda kwao Kigoma kuzikwa.
|
No comments:
Post a Comment