Mwili wa Mbunge Bilago kuagwa na Wabunge wote –Dodoma Leo May 29, 2018. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, May 29, 2018

Mwili wa Mbunge Bilago kuagwa na Wabunge wote –Dodoma Leo May 29, 2018.

Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Mwalimu Kasuku Bilago alifikwa na umauti wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jumamosi May 26, 2018,jijini Dar es Salaam. 

Mwalimu Bilago alizaliwa Tarehe 2/2/1964 na amefariki akiwa Mbunge wa kuchaguliwa wa Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma ambapo alichaguliwa mwaka 2015.
Naibu Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson akifungua kikao cha Bunge kwa kusoma dua, alitoa Bungeni hapo Taarifa ya Spika kuhusiana na msiba huo mzito uliolifika Bunge, na baade kutangaza kuahirisha Bunge hadi leo Jumanne May 29 saa tatu asubuhi, ili kupisha Maombolezo huku mipango ya kuuleta mwili katika viwanja vya Bunge kwa heshima za mwisho ikifanyika.

Mwili wa Marehemu Bilago unataraji kuletwa Bungeni leo May 29, 2018 kwa heshima za mwisho na baade kusafirishwa hadi Kijiji cha Kasuga Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ambako utahifadhiwa May 31, 2018.
Baada ya kuagwa Karimjee, mwili wa Marehemu Bilago utasafirishwa kwenda Dodoma ambapo Leo Jumanne May 29, utaagwa na wabunge wote, bungeni Jijini Dodoma kabla ya kusafirishwa kwenda kwao Kigoma kuzikwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad