Taswira Real Madrid wakibeba kombe la Klabu Bingwa Ulaya mara 3 Mfululizo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, May 27, 2018

Taswira Real Madrid wakibeba kombe la Klabu Bingwa Ulaya mara 3 Mfululizo.

Shabiki wa Liverpool Pichani Juu na Chini akisikitika kwa machungu baada ya kushuhudia uwanjani May 26, 2018 kilichowapata Liverpool kwa kukubali kipigo cha mabao 3 kwa 1kutoka kwa Real Madrid.
Mchezo huo wa Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu wa 2017/2018 uliipa Real Madridi Ubingwa huo dakika ya 51 kwa uzembe wa mlinda lango wa Liverpool Loris Karius ulimfanya Karim Benzema kuwapa Madrid bao la uongozi, bao hilo ni la 56 kwa Benzema na anakuwa mchezaji wa pili wa Kifaransa kufunga katika fainali ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya Zinedine Zidane.


Dakika ya 55 Sadio Mane aliisawazishia Liverpool na hili likiwa bao lake la 10 katika Mashindano haya ya Klabu Bingwa Ulaya msimu huu na la 20 kwa msimu huu, ambapo dakika ya 61,Kocha  Zinedine Zidane alimnyanyua Gareth Bale aliyekuwa benchi na Gareth Bale alifunga mabao mawili, na mabao ya Bale yanamfanya kuwa mchezaji wa kwanza kuingia kama sub na kufunga mara mbili  na kuufanya mchezo kumalizika kwa Real Madrid kuibuka kidedea kwa mabao 3-1 huku Zinedine Zidane akiwa kocha wa kwanza kubeba Ubingwa wa Ulaya mara tatu mfululizo.


Real Madrid wanakuwa timu ya kwanza kubeba kombe la Klabu Bingwa Ulaya  mara 3 mfululizo baada ya Bayern Munich 1974-1976, na timu za Uingereza sasa zinakuwa zimepoteza katika fainali 7 za mwisho za Ulaya dhidi ya timu kutoka Hispania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad