Kundi D Kuipa Yanga SC Ubingwa wa Kombe Shirikisho Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 21, 2018

Kundi D Kuipa Yanga SC Ubingwa wa Kombe Shirikisho Afrika.

Katika Droo ya hatua ya makundi iliyopangwa leo April 21, 2018 mjini Cairo, Misri iliongozwa na Katibu Mkuu wa CAF, Amr Fahmy na Katibu Msaidizi, Anthony Baffoe. ,Yanga SC ya Tanzania itaanzia ugenini hatua ya makundi kwa kumenyana na USMA Alger nchini Algeria Mei 6,2018 kabla ya kumenyana na Rayon Sport mjini Dar es Salaam Mei 16,2018 na itakamilisha mechi za mzunguko wa kwanza kwa kuwafuata Gor Mahia mjini Nairobi Julai 18,2018.

Mzunguko wa pili Yanga SC itaanzia nyumbani Julai 29,2018 na Gor Mahia, kabla ya kuwakaribisha na USMA Alger Agosti 19,2018 na kwenda kumalizia ugenini Agosti 29,2018 na Rayon.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad