Kijana Anthony akiwa na Baba yake
Mzazi.
Mwanafunzi
wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Ngundusi wilaya ya Ngara mkoani
Kagera amemtishia baba yake kumfikisha kituo kidogo cha Polisi Kabanga wilayani
humo akizuia kuuzwa kwa shamba la familia yao.
Mwanafunzi huyo Anthony Petro (10) amekuwa
jasiri kumzuia baba yake asiuze shamba baada ya kuona akisaini barua ya
mauziano na mtu aliyemfahamu akidai anaitwa Misheli, Kiongozi wa Kanisa
Katoliki Kigango cha Ngundusi Kata ya Kabanga wilayani Ngara.
Taarifa za
mwanafunzi huyo kupinga uamuzi wa baba yake zilianza kusambaa wiki iliyopita
kupitia video ya makundi ya mtandao wa WhatsApp akiibua hoja na hisia ya kutaka
kufahamu undani wake kwa kutumia Polisi wa Kabanga.
|
Akizungumza
Machi 11,2018 nyumbani kwa baba yake katika kijiji cha Ngundusi Kata ya
Kabanga, mtoto huyo alisema aliamua kuzuia kuuzwa shamba ili yeye na ndugu zake
wawili wa kike wasikose sehemu ya kuishi.
Alisema
nyumbani wanaishi maisha ya dhiki na taabu wakitegemea baba yao mzee anayefanya
shughuli za kilimo lakini akienda mitaani kuokota chupa za plastiki na kuziuza
ili akapate fedha ya chakula.
"Alitaka
kuuza shamba ili sisi tukaishi wapi, na tukalime wapi au tutatunzwa na
nini?" Alihoji na kuongeza " Nikitoka shuleni nakuja mjini kabanga
hadi kobero kutafuta misaada ya hela nikanunue unga wa kula na wadada
zangu"
Katika
familia ya mtoto huyo iliyo mbali na makazi ya watu, ina maisha duni kwani
watoto wanategemea kuokoteleza chupa na madumu ya plastiki na kuwauzia
watengenezaji wa pombe za asili wakitembea mpaka mji wa Kobero nchini Burundi
kuuza chupa na madumu hayo
Pia Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi Ngundusi, Mwl.Josia Cleophace alisema mwanafunzi Anthony si
mzuri sana kitaaluma kwani mahudhurio yake ni wastani anakuwa akienda kwenye
vibanda vya wafanyabiashara kuomba misaada ili kupata chakula cha familia
|
Alisema
anasoma darasa la kwanza lakini dada zake wawili wanasoma darasa la pili
wakipishana miaka baada ya yeye kuugua muda mrefu na kudumaa na zaidi
alisumbuliwa na funza kwa maana baba yake ni mzee hivyo alishindwa kumsaidia
kimazingira
“Baada ya kugundua hali ya familia
tulimchangia Sh15,000 akanunua dawa ya kuoshea mifugo na mafuta ya mgando kisha
kupona funza na amekuwa darasa la awali miaka miwili” Alisema Mwalimu
Josias
Aliyedaiwa
kununua shamba Michael Nazali ( Misheli) amekana kutohusika katika manunuzi ya
hivi karibuni ispokuwa mwaka 2000 ndipo alinunua sehemu yenye ukubwa wa hatua
20 kwa 50 na kwamba hujitokeza kumsaidia kutokana na ugumi wa maisha yake na
familia.
|
Alipohojiwa
maisha yake Mzee Petro Magogwa alisema amekuwa dhaifu baada ya kufiwa na wake
zake wawili huku wawili wakiachika kati yao watatu walitoka Burundi ambapo
wawili walio hai waliondoka na watoto wake watatu
Pia alisema
anao watoto watatu wa kike wameishaolewa na kuzaa wajukuu lakini pia
hawakujaliwa kupata familia imara kiuchumi hivyo anapougua au kuuguza msaada
wake ni kukata sehemu ya shamba na kuuza huku akitembeza chupa za plastiki
"Watengeneza pombe wananipatia Sh500 kwa
chupa 24 wakati mwingine kwa siku napata Sh 2000 nanunua unga wanangu wasilale
njaa" Alisema huku akibubujikwa machozi.
Alisema
anaishi kwa mara ya mwisho aliuza sehemu ya shamba miaka mitatu iliyopita baada
ya kuugua muda mrefu na watoto wake kwa thamani ya Sh120, 000 na alitumia kununua
mahitaji na dawa.
|
Mzee huyo
anao watoto watatu anawalea ambao ni Eliza Petro (9), Editha (13) wote darasa
la pili akiwemo Antony na amejaliwa kuoa wanawake wanne na kuzaa watoto 19
lakini tisa walipoteza maisha kwa nyakati tofauti.
Mke wa
kwanza walizaa watoto wanane wakafariki watano wa kiume na kubaki watatu wa
kike wote waliolewa mmojawapo yupo Burundi aliondoka na Mama yake ambapo mke wa
pili mtanzania alizaa watoto wanane kati yao saba wakafariki na kabaki mmoja
msichana anayeishi wilayani Kahama.
Alisema mke
wa watatu naye raia wa Burundi alizaa naye watoto watano na wawili wa kiume
walifariki na kubaki watatu wa kike nao baada ya mama yao kufariki
walichukuliwa na mama zao wadogo pamoja na wajomba pia wanaishi nchini Burundi.
|
Baada ya mke
wa tatu aliyezaa naye watoto wanne wawili wa kiume na wawili wa kike kufariki
kwa kuangukiwa na ukuta wa nyumba , mtoto wa kiume alifariki baada ya miezi
minane na kubaki na hao waliopo akiwemo huyo Anthony anayetetea ndugu zake
akizuia shamba kuuzwa.
“Bahati yangu mbaya na watoto wa kiume miaka
miwili ilipita nilioa mke mwingine wa nne na kuzaa naye mtoto mmoja wa kiume,
mtoto huyo alifariki na mama yake kuondoka na kubaki na hawa mnaowaona ila sina
nguvu za kuwatunza” Alisema Petro Magogwa
Mkuu wa
kituo cha polisi Kabanga wilayani Ngara Benadi Masakia amekiri kupokea taarifa
za Anthony kuzuia baba yake kuuza shamba pia ameshirikiana na askari wenzake wa
polisi jamii kumsaidia mzee Petro Sh 35,000 ili akawanunulie chakula na sabuni
watoto wake.
Na Shaaban
Ndyamukama, Radio Kwizera FM-Ngara/Kagera.
|
No comments:
Post a Comment