Askofu Niwemugizi aongoza Mazishi ya Padri Mutabazi mjini Rulenge. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, March 29, 2018

demo-image

Askofu Niwemugizi aongoza Mazishi ya Padri Mutabazi mjini Rulenge.

.com/simgad/
29746298_1810550518984850_1851715251_o
Askofu wa Jimbo la Rulenge-Ngara Muhashamu Severine Niwemgizi  akiwaongoza Mamia ya waumimi wakatoliki na wasio wakatoliki  wakati wa ibada ya mazishi ya aliyekuwa Paroko msaidizi wa Parokia ya Chato Jimbo Katoliki la Rulenge-Ngara Mosinyori Emmanuel Mutabazi yaliyofanyika March 27,2018 katika makabuli ya Mapadre mjini Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera.
29747062_1810550505651518_2112071885_o

29746737_1810550525651516_1884511006_o
Akitoa Mahubiri katika ibada hiyo ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa Katoliki mjini Rulenge, Askofu wa Jimbo la Rulenge-Ngara Muhashamu Severine Niwemgizi amesema Jimbo hilo limepata pigo la kuondokewa na Mosinyori Mutabazi kwani jimbo lilikuwa likimtegemea kama mtafsiri wa biblia

Askofu Niwemugizi amesema Mosinyori Emmanuel Mutabazi katika kipindi chote cha miaka 48 ya utume wake amekuwa akifanya kazi kwa bidii huku akiwaheshimu wakubwa na wadogo.
29883708_1810550515651517_773753181_o
Hawa Masista ni Ndugu wa Marehemu Mosinyori Emmanuel Mutabazi waliposhiriki kuweka shada la maua wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Juzi March 27,2018 katika makabuli ya Mapadre mjini Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera.
29831354_1810550512318184_944504798_o

29681387_1809351249104777_439272510_o

29693447_1809351239104778_1738140309_o
Kwa upande wao waumini waliojitokeza kuuga mwili wa Mosinyori Mutabazi wamesema wamempoteza mtu muhimu sana katika kanisa kutokana na wataendelea kumuenzi na kumuombea kwa yote mema ambayo aliyafanya kwa maendeleo ya kiroho.

Mosinyori  Emmanuel Mtabazi alikuwa mtaalam wa kutafsiri biblia takatifu na Paroko msaidizi wa Parokia ya Chato mkoani Geita ambaye alifariki alfajiri ya Marchi 25,2018.

Mosinyori Emmanuel Mtabazi enzi za uhai wake amewahi kuwa mkufunzi katika chuo kikuu cha Kweya Nairobi nchini Kenya na amekuwa katika utume wake kwa kipindi cha miaka 48.
29693648_1809351229104779_1411149033_o

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *