Akiongea na
wananchi katika Kituo cha Afya Nyakanazi Wilayani Biharamulo Mkuu wa Mkoa Kijuu
alisema kuwa alifika kituoni hapo pamoja na Vituo vingine vya Afya ambavyo
vimepewa fedha na Serikali ili vikarabatiwe ili ajionee kama fedha hizo
zinatumika ipasavyo ikiwa ni pamoja na michango ya wananchi wa eneo husika na
kuhakikisha ujenzi unakamilika ifikapo Machi 30, 2018.
Serikali
imetoa kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kwa vituo vinane katika Mkoa wa Kagera
ambapo awamu ya kwanza ilitolewa shilingi milioni 500 kwa kila kituo Vituo vya
Nyakanazi (Biharamulo) na Kayanga (Karagwe). Awamu ya pili Serikali ilitoa
shilingi milioni 500 kituo cha Katoro (Bukoba) na Vituo vya Kishanje (Bukoba),
Mabawe na Murusagamba (Ngara), Kimea (Muleba), na Murongo (Kyerwa) vilipewa shilingi
milioni 400 kila kimoja.
Akitoa
ufafanuzi Mkuu wa Mkoa Kijuu kwenye Mikutano ya hadhara na wananchi
alipotembelea na kukagua ukarabati wa Vituo vilivyopata fedha kutoka Serikalini
alisema kuwa Vituo hivyo vilipata fedha katika awamu ya kwanza kutokana na
juhudi za wananchi wenyewe katika maeneo husika kuonesha juhudi katika
uchangiaji wa ujenzi wa Vituo vyao vya Afya.
|
Mkuu wa Mkoa
Kijuu aliwahamasisha wananchi katika maeneo mengine ambayo vituo vyao
havijapata fedha kutoka Serikalini kuendelea kuchaangia ujenzi wa Vituo na
Zahanati ili majengo na miundombinu yote inayotakiwa ikamilike, kupitia juhudi
hizo za wananchi Serikali pia itaweza kuchangia fedha kwa maeneo yale ambayo
wananchi wataonesha juhudi za kuchangia maendeleo yao.
Katika ziara
hiyo Mkuu wa Mkoa alisistiza mambo makuu manne kama ifuatavyo, Kwanza, Vituo
vya Afya vilivyopata fedha za Serikali zitumike kwa kusimamiwa na Kamati za
Vituo pia watumike mafundi wa eneo husika bila kuwatumia Wakandarasi na
Wakandarasi washauri katika ujenzi ili kuepuka gharama kubwa za ujenzi aidha,
ujezi uzingatie viwango kwa usimamizi wa Wahandisi wa Halmashauri.
Pili, Mkuu
wa Mkoa aliwaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanatenga
na kuyapima maeneo ya Vituo vya Afya na Zahanati kwa manufaa ya upanuzi wa
baadae na kuondoa migogoro na wananchi jirani. Tatu, wananchi wanatakiwa
kuendelea kujishughulisha na kilimo ili kujipatia chakutosha na kuchangia
maendeleo yao kama ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya.
Nne,
wananchi, Taasisi za Serikali na zisizokuwa za Serikali zinatakiwa kupanda miti
ya matunda kuzunguka maeneo ya Taasisi hizo na wananchi wapande miti ya matunda
ya aina mbalimbali isiyopungua mitano kuzunguka kaya zao ili kupunguza tatizo
la utapiamlo katika Mkoa wa Kagera ambalo linatokana na wananchi wa Kagera
kutokula matunda na mchanganyiko sahihi wa vyakula.
|
Katika hatua
nyingine kwenye ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa Dk.
Thomas Rutachunzibwa ambaye alipata fursa ya kuwaelimisha wananchi juu ya
miundombinu inayotakiwa katika Vituo vya Afya na Zahanati ambapo ili kituo cha
Afya kiitwe Kituo cha Afya kinatakiwa kuwa na miundombinu ifuatayo:
Kituo cha
Afya kilichokamilika na kuruhusiwa kutoa huduma kwa wananchi kinatakiwa kuwa na
Jengo la Wagonjwa nje na wagonjwa wa ndani, Jengo la Maabara, Wodi ya
akinamama, Jengo la upasuaji, Wodi nyingine za wagonjwa, Vyoo vya watumishi na
wagonjwa, Nyumba za watumishi wawili, Kichomea taka, Maji ya kutosha, Nishati
ya umeme na Nyumba ya kuhifadhia maiti.
Dk. Rutachunzibwa
aliwakumbusha wananchi katika ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa kuwa kwa sasa Serikali
imetoa ramani ya ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati ambapo wananchi
wanatakiwa kuzingatia ramani hizo wakati wa ujenzi ili majengo ya kutolea
huduma za afya yakidhi viwango.
Picha/Habari
Na: Sylvester Raphael
|
No comments:
Post a Comment