Yanga SC na Pointi 28 Baada ya Azam FC kufungwa Nyumbani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 27, 2018

Yanga SC na Pointi 28 Baada ya Azam FC kufungwa Nyumbani.

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara Yanga ya Dar es Salaam Wakiwa ugenini katika uwanja wa Azam Complex, Mbande Chamazi kucheza mechi yake ya 15 Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya wenyeji wao Azam FC.- imeibana Azam FC na kuichapa kwa mabao 2-1 ushindi ambao umeipa Yanga pointi tatu na kuifanya ifikishe pointi 28 na kubaki nafasi tatu ikiwa ni tofauti ya pointi mbili na Azam ambayo ina pointi 30 katika nafasi ya pili huku ikiwa nyuma ya Simba SC kwa Pointi nne.

 Ushundi wa Yanga SC umekuja wakati timu hiyo ikikabiliwa na idadi kubwa ya wachezaji wenye majeraha (Yohana Mkomola, Pato Ngonyani, Thabani Kamusoko, Amis Tambwe, Donald Ngoma, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Pius Buswita ambaye alikuwa anatumikia kadi tatu za njano).

Mechi nyingine za Ligi Kuu leo January 27, 2018, Mwadui FC imelazimishwa sare ya 2-2 na Njombe Mji FC Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga, Mbeya City imelazimishwa sarte ya 0-0 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya na Kagera Sugar imetoka 0-0 na Lipuli FC Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad