Magunia 300 ya Bangi yateketezwa Arusha. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 27, 2018

Magunia 300 ya Bangi yateketezwa Arusha.

Polisi wakifanya kazi ya kuteketeza magunia ya Bangi.

Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kwa kushirikiana na jeshi la polisi, wamefanya oparesheni ya kukamata na kuteketeza magunia ya bangi zaidi ya mia tatu, Mkoani  Arusha, huku ikiwakamata na kuwafungulia kesi watuhumia 18 kwa kukutwa na dawa hizo.

 Katika zoezi la uchomaji  wa magunia hayo, Kamishina  wa sheria mamlaka ya kupambana na kudhibiti dawa za kulevya, Edwin Kakolaki, amesema dawa hizo ni kutokana na msakao uliofanyika kwa nyakati mbalimbali mkoani Arusha,  na wameziteketeza kwa mujibu wa sheria namba tano ya mwaka 2015 ya ku.

Licha ya kubainisha kupungua kwa kiwango kikubwa cha matumizi ya  dawa za kulevya hapa nchini, Kakolaki amesema baadhi ya waingizaji wamebuni mbinu mpya ya kuingiza dawa aina ya kokeni na heroini na serikali inaendelea kuwadhibiti.

Mpaka sasa zaidi ya waraibu 5000 wanapatiwa matibabu ili kuachana kabisa na matumizi ya dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad