Picha za
tukio hilo zinaonyesha eneo kubwa la daraja hilo lenye urefu wa mita 450 likiwa
limeanguka. Waziri wa Usafirishaji Germán Cardona alisema chanzo cha ajali hiyo
kinachunguzwa.
Mfanyakazi mmoja miongoni mwa waliojeruhiwa alisimulia tukio
hilo na kusema:- “Kila mtu alianza kupiga kelele kuwa
daraja linaanguka, sikuwa na muda wa kufanya chochote na kisha nikasikia kitu
kinanipiga kichwani,”
|
Daraja hilo
ni sehemu ya mpango mkubwa wa kuendeleza njia inayoelekea Bogota katika mbuga
za mashariki ili kuifanya iwe na njia mbili.
Kazi iliyopangwa inajumuisha
ujenzi wa njia 18 za ndani ya milima, madaraja 42 pamoja na kamera za kurekodi
matukio.
Njia iliyopo
ambayo ni nyembamba hufungwa kila mara kutokana na malori yanayopeleka mizigo
Bogota yanapoharibika na kukwamisha magari mengine kupita.
|
No comments:
Post a Comment