Rais Magufuli aomboleza Vifo vya Watu 11 , Biharamulo,Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 15, 2018

Rais Magufuli aomboleza Vifo vya Watu 11 , Biharamulo,Kagera.

Ajali iliyohusisha magari matatu huko Biharamulo, Kagera.

Watu kumi na mmoja wamekufa na wengine watano wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari matatu ikiwemo gari dogo la kubeba abiria na malori mawili iliyokuwa yakitokea wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Olomi amethibitisha kutokea ajali hiyo na tayari Rais  John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu kufuatia ajali hiyo.

Ajali ambayo imeacha simanzi kubwa miongoni mwa ndugu na familia ukiwa ni muendelezo wa ukosefu wa umakini kwa madereva pindi wanapokuwa barabarani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, SACP Olomi amethibitisha idadi ya vifo pamoja na majeruhi waliotokana na ajali hiyo inayodaiwa kusababishwa na mwendo kasi.

Kamanda huyo amesema, gari hilo la abiria lilikuwa na jumla ya abiria 17 na kati ya hao 11 wamekufa na watano wameruhiwa na wanaendela kupatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya Biharamuro.

SACP Olomi amesema, chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa gari la abiria ambaye anadaiwa hakutumia akili kwa kutaka kulipita gari la mbele yake bila kuwa makini na hivyo kukutana uso kwa uso na lori .  

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewakumbusha watumiaji wa barabara hasa madereva kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani na ameviagiza vyombo vinavyohusika kuongeza jitihada za kukabiliana na ajali za barabarani ili kuokoa maisha ya watu na mali zinazopotea kutokana na ajali. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad