Source: RK, Ak (damu)
Ed: AG
Date: Monday, January 15,
2018
BUKOBA
Wakazi mkoani Kagera wametakiwa
kujenga tabia ya kujitokeza kuchangia damu katika vituo mbalimbali vya kutolea
huduma ya damu mko ili kuokoa maisha ya wananchi wanaopoteza maisha kutokana na
kupungukiwa damu
Hayo yameelezwa na makamu mwenyekiti
wa umoja wa wanawake waombaji kanda ya ziwa Bi.Christina Mwainunu wakati
akizungumza na redio kwizera baada kikundi chake kujitokeza katika hospitali ya
rufaa ya mkoa wa Kagera kutoa damu
Amesema kuwa kilichowasukuma kutoa
damu ni kutokana na kusikitishwa na taarifa za wanawake, watoto na watu wengine
wanaopoteza maisha kwa kukosa damu
Insert……..Christina
Mwainunu
Cue
in…….
Cue
out…...
Kwa upande wake kiongozi wa timu ya kukusanya
damu mkoani Kagera Bw.Amos Mashweka amewapongeza wanawake hao kwa kuona umuhimu
wa kuchangia damu ili kunusuru maisha ya wagonjwa na kuitaka jamii kuendelea kujitokeza
kuchangia damu
Source: RK, JOVIN (ajari yaua
watu 11)
Ed: AG
Date: Monday, January 15,
2018
BIHARAMULO
Watu wawili wamefariki wakati
wakiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali teule ya wilaya ya Biharamulo na
kufikisha idadi ya watu 11 kufuatia ajali ya gari iliyotokea jana katika kijiji
cha Mugera kata ya Nyantakara wilayani Biharamulo mkoani Kagera
Mganga mkuu wa hospitali teule ya
wilaya ya Biharamulo Dr. Gresimus Sebuyoya amesema kuwa majeruhi waliofikishwa
hospitalini walikuwa saba lakini wawili walifariki muda mfupi kutokana na
kuvuja damu nyingi
Aidha amesema kuwa watu tisa
walifariki papo hapo mara baada ya ajali kutokea majira ya saa kumi za jioni na
majeruhi watano waliobakia wanaendelea kupatiwa matibabu
Insert….Dr
Sebuyoya
Cue
in…..
Cue
out…..
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera
Augustino Olomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyohusisha Haice yenye
namba za usajiri T542 DKE iliyogongana na magari makubwa matatu yenye namba za
usajiri T 147 DUJ, T 860 CGS na T 103 CGS
Source:
RK, em (Uhaba wa matundu ya vyoo)
Ed: AG
Date: Monday, January 15,
2018
KARAGWE
Mwalimu mkuu
wa Shule ya msingi Runyaka iliyoko wilayani Karagwe Mkoani Kagera Bw Desdery
Costantine amesema shule inahitaji matundu mapya 30 ya vyoo ili kufunga matundu
20 yaliyopo kwa sasa kwani yanakalibia kujaa
Bw Costantine
amesema kuwa shule hiyo yenye wanafunzi 722 huenda ikakumbwa na magonjwa ya
mlipuko ikiwa hatua za dharura hazitachukuliwa kwani hata mwitikio wa wananchi
kuchangia miundombinu ya shule ni mdogo kutokana na sera ya elimu bila malipo
Insert………………Bw Costantine
Cue in……………….Kwa sasa
Cue Out………….vyoo
Nao baadhi ya
wanafunzi wa shule hiyo wamesema kuwa kutokana na vyoo hivyo kujaa
wanasumbuliwa na harufu chafu inayokuwa ikitoka kwenye vyoo hivyo kwani hata
wakifanya usafi hakuna unafuu wanaoupata
Hivi Karibuni
mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe Bw Wallence
Mashanda akizungumza na wandishi wa habari, aliwataka wananchi kusaidiana
na Serikali kuboresha miundo mbinu ya shule ili wanafunzi waweze kuyafurahia
masomo yao
Source: RK, LT (Wizi)
Ed: AG
Date: Monday, January 15,
2018
KINSHASA
Kiongozi wa soko kuu katika mji wa Baraka nchini Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo amewataka vijana kuachana na tabia ya kuiba mbao ambazo
zimejenga vibanda pamoja na meza za biashara kwani ni kurudisha nyuma maendeleo
ya soko hilo
Bw. Alenga Muhochu amesema wapo vijana wanaoiba mbao na miti
ndani ya soko kwa lengo la kuwasha moto nyakati za usiku kwenye misiba hivyo
ameiomba serikali kuingilia kati swala hilo
Insert…..ALENGA
Cue In: ndio
wanakuja kuvunja soko…
Cue Out…sikitiko
langu ni hilo.
Kwa upande wake mkuu wa sekta ya Mutambala Bw. Luhanusha
Josué amekemea vikali hatua hiyo ya vijana kujihusisha na vitendo vya wizi na
kwamba serikali itawachukulia hatua kali wale watakaokamatwa wakiiba
Aidha Bw. Luhanusha amesema soko ni moja kati ya vitega
uchumi vya serikali na linasaidia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya mji, hivyo
ameagiza uongozi wa jeshi la polisi tarafa ya Fizi kupanga askari watakao
husika na ulinzi nyakati za usiku kwenye soko hilo
No comments:
Post a Comment