Katibu
Tawala Wilaya ya Sengerema, Alen Augustine alisema kazi ya kukamata shehena
hiyo ilifanikiwa baada ya vyombo vya dola kupata taarifa kutoka kwa raia wema
kuhusu mipango ya kusafirisha samaki hao kwenda nje ya nchi kinyume cha sheria.
“Katika
zoezi hilo, pia tumefanikiwa kukamata nyavu 012 za kuvuli samaki zenye matundu
ya nchi 4.5 na sita zenye thamani ya Sh 22.9 milioni,” alisema Augustine.
|
Kaimu Ofisa
Uvuvi, Halmashauri ya Sengerema, Benerdictor Magaonda aliahidi kuwa ofisi yake
itaendelea kuwasaka na kuwatia mbaroni wote wanaojihusisha na uvuvi haramu na
biashara ya samaki bila kuzingatia sheria.
Ofisa
Mtendaji Kata ya Nyamapande, Wiliam Donart aliwaomba wananchi kushirikiana na
Serikali katika mapambano dhidi ya uvuvi na biashara haramu ya Samaki.
Alisema
mapambano hayo yatasaidia kulinda rasilimali hiyo kwa faida ya vizazi vya sasa
na vijavyo.
|
No comments:
Post a Comment