Vijana 57 wamehitimu Mafunzo Mgambo , Kata ya Bukiriro wilayani Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 15, 2017

Vijana 57 wamehitimu Mafunzo Mgambo , Kata ya Bukiriro wilayani Ngara.

Vijana 57 wamehitimu mafunzo ya jeshi la akiba yaani Mgambo katika Kata ya Bukiriro wilayani  Ngara mkoani Kagera  hii Leo November 15,2017 kwa lengo la kuimarisha Ulinzi na Usalama.

Kati ya vijana hao 10 ni wa kike na mafunzo yalianza June 5 mwaka huu katani humo ambapo yamefungwa na Mkuu wa wilaya ya Ngara, Luteni kanali Michael Mntenjele .
Luteni Kanali Michael Mntenjele ( wa pili kutoka kulia pichani ) amewakata wahitimu hao wa Mgambo kuimarisha amani na utulivu kwa kudhibiti magendo maeneo ya mpakani na kushirikiana na vyombo vya dola kutokomeza uhalifu.

Vijana hao wamesema katika mafunzo yao wamekumbana na changamoto za kutambua uzalendo, kujiandikisha wasiokuwa RAIA kutoka kata jirani ambao baada ya kuchujwa wamebaki watanzania watakaootumikia taifa kwa weledi mkubwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad