Mshindi wa Big Brother Hotshots 2014, Idris Sultan,
akiwa kwenye pozi.
|
Meneja Uhusiano wa Multchoice Barbara Kambogi
(kushoto),akiwa na Idrisa (katikati) na Meneja Masoko wa
Multichoice, Furaha Samalu, katika meza kuu.
|
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kwenye tukio
hilo.
Mshindi wa Big Brother Hotshots,
Mtanzania Idris Sultan, hivi sasa anafikiria zaidi maisha yake ya baadaye
badala ya kufikiria fedha alizopata katika shindano hilo lililomalizika hivi
karibuni Afrika Kusini.
Alisisitiza
kuwa ataendelea kuwasaidia vijana walio katika changamoto mbalimbali ikiwa ni
pamoja na kupiga vita madawa ya kulevya, mimba za utotoni na mengineyo.
Hayo
ameyasema Jana Desemba 11,2014, jijini Dar es Salaam baada ya kuwasili
jana kutoka Afrika ya Kusini na kulakiwa na Watanzania katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere akiwa na maofisa wa kampuni ya Multchoice
Tanzania.
Akizungumza
pia katika hafla hiyo, Meneja Uhusiano wa Multchoice, Barbara Kambogi, amesema
Idris atakuwa chini ya kampuni hiyo kwa miezi kadhaa na kufanya naye kazi
katika miradi mbalimbali.
Idris alitoa shukrani nyingi kwa Watanzania na Waafrika kwa ujumla kwa kumpigia kura iliyomwezesha kushinda kitita Dola 300,000 za Marekani.Kujua mengi tembelea www.globaltvtz.com
(Habari/Picha:
Gabriel Ng’osha/GPL)
|
UNGANANASI
KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
No comments:
Post a Comment