Simba ilipocheza na
Azam FC kwa mara ya kwanza katika dimba la Chamazi, Dar Es Salaam.
Mechi ya
ligi kuu Tanzania bara kati ya Yanga SC vs Tanzania Prisons, na mechi kati ya
Simba SC vs Lipuli FC zilizopangwa kuchezwa tarehe 25 na 26 mwezi huu, sasa
zitapigwa katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi badala ya Uwanja wa Uhuru kama
ilivyokuwa imepangwa awali.
Taarifa
iliyotolewa na bodi ya ligi imesema kuwa sababu ya kuhamisha mechi hizo ni
mmiliki wa Uwanja wa Uhuru (Serikali) kuutumia uwanja huo kwa shughuli nyingine
za kijamii kuanzia tarehe 24 hadi 27 mwezi huu.
Mechi zote
za raundi ya 11 zitakazopigwa wikiendi ijayo ziko kama ifuatavyo.
Ijumaa ya
tarehe 24, Novemba utapigwa mchezo mmoja ambapo Ndanda FC itakuwa nyumbani
kuwakaribisha Njombe Mji.
Jumamosi ya
tarehe 25, Novemba, kutakuwa na mechi tano kama ifuatavyo:-
Yanga SC vs
Prisons
Singida
United vs Mbeya City
Mbao FC vs
Mwadui
Kagera Sugar
vs Stand United
Ruvu
Shooting vs Majimaji FC
Jumapili ya
Novemba 26 ni mechi moja itakayowakutanisha vinara wa ligi hiyo, Simba SC
watakaowakaribisha Lipuli FC na Jumatatu ya Novemba 27, Azam FC watakuwa
wenyeji wa Mtibwa Sugar, mchezo utakaopigwa Chamazi Dar es Salaam saa 1:00
usiku.
|
No comments:
Post a Comment