Mchezaji Ibrahim Ajib ameendelea kuwasha moto akiwa na Timu yake ya Yanga SC baada ya leo
Jumapili October 22, 2017 kuifungia mabao mawili Timu yake kwenye ushindi wa 4-0
dhidi ya Stand United na kuifanya Yanga SC ifikishe pointi 15 sawa na Simba
SC na Mtibwa Sugar.
Simba SC na Mtibwa Sugar zilifikisha alama 15 baafa ya kushinda michezo yao
ya jana kwa Simba SC 4-0 dhidi ya Njombe Mji FC lakini ushindi wa Yanga SC leo unafanya timu tatu kufungana pointi
lakini tofauti ya magoli ndio unazitofautisha katika msimamo wa ligi.
Ajib ndio anaongoza kwa ufungaji kwenye kikosi cha Yanga akiwa na magoli matano (5) aliyoyafunga kwenye mechi saba alizocheza.
Ajibu yupo nyuma ya Emanuel Okwi kwenye orodha ya wafungaji VPL 2017/2018, Okwi
amefunga magoli nane (8), Ajib magoli matano (5) na Mohamed Rashid wa
Tanzania Prisons mwenye magoli manne (4).
Yanga SC ilikuwa haijashinda mechi kwa zaidi ya magoli mawili, huu ni
ushindi wao mkubwa Tangu kuanza kwa VPL msimu huu.
Walifunga goli moja
mfululizo kwenye mechi zao nne za kwanza kabla ya kupata ushindi wa
magoli 2-1 walipocheza dhidi ya Kagera Sugar mchezo uliopita.
|
No comments:
Post a Comment