Mchezaji Cristiano
Ronaldo (kulia) alishangilia akiwa na wenzake Gareth Bale baada ya kufunga bao la pili la
Real Madrid dakika ya 49 katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji, Borussia
Dortmund kwenye mchezo wa Kundi H wa Ligi
ya Mabingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Signal Iduna Park mjini Dortmund.
Bale aliyetoa pasi la bao la pili, ndiye
aliyefunga bao la kwanza dakika ya 18, wakati Ronaldo alifunga na la tatu pia
dakika ya 79 na Pierre-Emerick Aubameyang akawafungia wenyeji la kufutia
machozi dakika ya 54.
|
Kufunga
magoli mawili kwa Cristiano Ronaldo kunamfanya kuzifunga timu za Ujerumani kwa mara ya 25
akicheza dhidi yao kwa mechi 21, hata hivyo usiku huo umemfanya Ronaldo
kufikisha jumla ya game 400 akiichezea Real Madrid akiwa kafunga jumla ya
magoli 411, assist 111 na amefunga jumla ya hat-trick ya 42.
MSIMAMO WA KUNDI H.
|
MATOKEO YA MECHI ZINGINE JANA. |
No comments:
Post a Comment