Mabingwa
watetezi wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wamelazimishwa sare ya 0-0 dhidi ya Arsenal
katika mchezo wa vuta nikuvute uliochezwa leo September 17,2017 kwenye uwanja
wa Stamford Bridge.
|
Tukio kubwa
zaidi kwenye mchezo huo, ni kupewa kadi nyekundu kwa beki wa Chelsea David Luis kunako dakika ya 86 baada ya
kumchezea rafu beki tatu wa Arsenal Sead
Kolasinac.
|
Baadhi ya
wachambuzi wakiwemo Alan Shearer na Peter Schmeichel wamepata kigugumizi juu ya
kadi hiyo nyekundu huku wengi wao wakiamini kadi njano ingekuwa uamuzi sahihi.
|
Mchezo huo uliojaa ufundi wa kila namna, pia ulitawaliwa na ubabe mwingi na kumpelekea mwamuzi Michael Oliver kutoka kadi za njano mbili kwa Chelsea na tatu kwa Arsenal. |
No comments:
Post a Comment