Emmanuel Okwi katikati pichani akishangilia na
wachezaji wenzake wa Simba SC baada ya kufunga mabao mawili leo September
17,2017 dhidi ya Mwadui FC.
|
Mabao yote ya Simba leo yalikuwa
mazuri na yenye kudhihirisha uwezo binafsi wa wachezaji kufunga na kwa ujumla,
Wekundu wa Msimbazi walikuwa katika mechi nyepesi mno jioni hii.
|
Simba SC imewapa burudani ya nafsi mashabiki
wake leo September 17,2017 baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga katika mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
|
Mshambuliaji
wa Simba SC, John Bocco.
Nyota wa
mchezo wa leo kwa mara nyingine amekuwa mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyefunga mabao mawili
na kufikisha mabao matano katika mechi mbili tu za Ligi Kuu alizocheza msimu
huu, kufuatia kufunga mabao matatu katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mchezo wa kwanza.
|
Hapa chini Matokeo ya Mechi za Jana September 16,2017.
|
Msimamo wa VPL 2017/2018 Ulivyo sasa.
|
No comments:
Post a Comment