Wanafunzi Kagera waaswa Kudumuni katika Nidhamu ili kufikia Malengo Kielimu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, August 04, 2017

Wanafunzi Kagera waaswa Kudumuni katika Nidhamu ili kufikia Malengo Kielimu.

Mwenge wa Uhuru waendelea na mbio zake Mkoani Kagera ambapo tayari umezindua miradi 28 yenye thamani ya shilingi bilioni 8,438,723,915 kwenye Halmashauri za Wilaya tatu Biharamulo, Ngara na Karagwe na miradi hiyo 28 ni kati ya 66 itakayozinduliwa na Mwenge huo katika mkoa mzima ambapo jumla ya thamani ya miradi hiyo ni shilingi bilioni 20,003,692,230.

Mwenge wa Uhuru ukikabidhiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kutoka Wilayani Ngara jana tarehe 3 Agosti, 2017 Mwenge wa Uhuru umezindua miradi 4, umekagua miradi 3 na kuweka mawe ya msingi katika miradi 3 na kukamilisha jumla ya miradi 10 yenye thamani ya shilingi bilioni 2,694,851,845

Aidha, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka huu 2017 ,Bw.Amour Hamad Amour akizindua mabweni mawili ya wavulana katika Shule ya Sekondari Bugene yaliyojengwa kwa gharama ya shilingi 152 milioni fedha za Serikali Kuu, aliwaasa wanafunzi wa shule  hiyo yenye kidato cha tano na sita kusoma kwa bidii ili wayafikie malengo yao na malengo ya wazazi wao pia.

Bw. Amour alisema kuwa ili wanafunzi hao waweze kufaulu vizuri ni lazima wawe na nidhamu ya hali ya juu hasa kwa walimu wao wanaowafundisha pia kujiheshimu wao wenyewe na kuzingatia masomo na maadili wanayofunzwa shuleni hapo.

Pia Bw. Amour aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwafundisha wanafunzi kwa umakini mkubwa na kupelekea kupata matokeo mazuri ya kidato cha sita kwa mwaka 2017. 

Pia aliwasihi kuhakikisha wanazingatia maadili ya taaluma yao wanapokuwa wanawafundisha wanafunzi hao.
Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2017 alitoa angalizo kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bugene kuwa ni lazima kuangalia nidhamu za walimu wake na kuchukua hatua mapema kwa mwalimu atakayekwenda kinyume na maadili ya kazi yake kabla yeye Mkuu wa Shule hajachukuliwa hatua na Serikali ya awamu ya tano.



Naye Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Bw. Godfrey Mheruka akimshukuru Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 alisema kuwa uongozi wa Wilaya uliamua kupeleka Mwenge wa Uhuru katika Shule ya Sekondari Bugene baada ya shule hiyo kufanya vizuri katika matokeo yake ya kidato cha sita 2017 ambapo walifaulu kwa ( Daraja la I = 13, Daraja la II =41, Daraja la III =22 na Daraja IV =2 aidha hakuna mwanafunzi aliyepata sifuri)

Mwenge wa Uhuru tayari unaendelea na mbio zake Mkoani Kagera katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa leo tarehe 4 Agosti, 2017.

Habari/Picha Na: Sylvester Raphael

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad