Barabara
hiyo imeanza kuchimbika na lami kubanduka na kubaki vumbi licha ya kufanyiwa
ukarabati wakati wote wa kila mwaka.
Ubovu wake
ni kujaa mashimo yanayochangia magari yenye mizigo kushindwa kuendelea na safari,
huku mengine yakipinduka baada ya kupanda milima na hata kurudi nyuma.
|
Wakizungumza
na Mwandishi wa Mtandao huu katika eneo hilo, baadhi ya madereva
wamesema eneo hilo ni bovu miaka yote na unapofanyika ukarabati, wakandarasi
wanatumia saruji rojorojo bila kuzingatia kuwa magari yanayopita yanakuwa na
tani nyingi za mizigo.
Wamesema
magari hayo yanasafiri kutoka na kuingia Dar Es Salaam hadi
Rwanda na Burundi na hata Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, kwa
kuingiza fedha zinazoweza kuinua uchumi wa Taifa, hivyo
serikali ya Tanzania haina budi kujenga upya barabara hiyo, kutoka
Nyakanazi wilayani Biharamulo hadi Rusumo Wilayani ya Ngara mkoani
Kagera.
|
Kukwama kila
wakati kwa magari katika eneo hilo la Nyabugombe , safari za magari ya abiria
kutoka Ngara kwenda mikoani kupitia eneo la barabara hiyo zimekuwa zikisimama
kwa saa kadhaa huku huduma za kijamii kama maji, mighahawa ya kuuzia
chakula , zahanati na mawasiliano ya mitandao ya simu za mkononi vikikosekana
na kuleta changamoto kwa wasafiri.
Hata hivyo Mhandisi
wa barabara wa mkoa wa Kagera Bw.Chakindo
Nasiri, alipotafutwa kwa njia ya simu amesema barabara hiyo inahitaji
kujengwa upya, na kinachofanyika hivi sasa ni ukarabati mdogo ili kuwezesha
magari kupita kusafirisha bidhaa kuelekea nchi za Rwanda. Burundi na DRC.
Picha Na
Shaban Ndyamukama.
|
No comments:
Post a Comment