Kikao cha Ndani kilifanyika na Waziri Magembe.
|
Awali Waziri
wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne
Magembe ( Aliyesimama Pichani ) ameipongeza Idara ya Wanyamapoli mkoa wa Kagera kwa kufanikisha
operation ya kuondoa mifugo iliyokuwa ndani ya mapori ya akiba ya hifadhi ya Biharamulo,
Kimisi na Burigi na kwamba Serikali haitaruhusu tena mifugo hiyo kuingia ndani
ya hifadhi
Pro. Magembe amesema kuwa operation za mara kwa
mara zitakuwa zinafanyika katika mapori hayo ya hifadhi ikiwemo kurusha ndege
zenye rubani na zile zisizo na rubani ili kuhakikisha mifugo yote inaondolewa
lakini pia mifugo hiyo hairudishwi katika mapori hayo kama walivyozoea kufanya
siku za nyuma.
|
Kwa upande
wake Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mhe.Oscar
Mukasa akiwawawakilisha Wabunge wenzake wa Mikoa ya Kagera na Geita amesema
katika kikao na Waziri Mkuu walikubaliana Waziri wa Maliasili akutane na
kuzungumza na Wafugaji na kuwataka Wafugaji kuwa watulivu wakati Wabunge wao
wakiendelea kuwasiliana na Serikali.
|
Picha ya
Risiti wanazopewa Wanunuzi wa Mifugo.
|
Picha ya
Risiti wanazopewa Wanunuzi wa Mifugo.
|
Picha ya
Risiti wanazopewa Wanunuzi wa Mifugo.
|
No comments:
Post a Comment