Wabunge hao wakielekea mahali ambapo
magari hayo yalikuwa yameegeshwa.
Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi John Kijazi amekabidhi magari hayo aina ya Land Cruiser Hardtop
kwa niaba ya Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa Mbunge wa Nkasi Kaskazini Mkoa
wa Rukwa Mhe. Ally Keissy, Mbunge wa
Viti Maalum Mkoa waTabora Mhe. Munde
Tambwe na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Lucy Mayenga.
|
Mbunge wa
viti maalum CCM, Lucy Mayenga akikabidhiwa funguo za gari na Balozi John
Kijazi.
|
Mbunge wa
Nkasi (CCM), Ally Kessy akifurahia baada ya kukabidhiwa gari hilo.
Akizungumza
baada ya makabidhiano hayo, Balozi Kijazi amesema Mhe. Rais Magufuli ametoa
magari hayo baada ya kuguswa na kilio cha muda mrefu cha Wabunge hao waliokuwa
wakiomba wananchi wao wapatiwe magari ya wagonjwa.
“Mhe. Rais
ameamua kuwakabidhi nyinyi haya magari kutokana na vilio vyenu ambavyo amekuwa
akivisikia mara kwa mara, Mhe. Keissy umekuwa hata ukitafuta miadi ya kuja
kumuona Mhe. Rais kwa suala hili, Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakiyazungumza
haya kwa muda mrefu.
“Tunafahamu
kila Mbunge katika jimbo lake anahitaji kupata huduma kama hii, na huduma kama
hii ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, kwa hiyo sisi
Serikali kila tunapopata uwezo basi tunasaidia pale tunapoweza kufikia kwa
wakati ule, tulishatoa magari mengine matatu kama haya Chalinze na vituo
vingine vya Morogoro.” Amesema Balozi Kijazi.
Taarifa
Kamili ya Ikulu,soma hapa Chini.
|
No comments:
Post a Comment