Magoli ya Crystal
Palace yalifungwa na Andros Townsend
dakika ya 17, Yohan Cabaye dakika ya 63 na Luka Milivojevic kwa mkwaju wa
penati dakika ya 68.
|
Katika mchezo
huo ,Arsenal ilimaliza mchezo huo ikiambulia kumiliki mpira kwa asilimia 73 na
Crystal Palace 27 na kipigo hicho kinaifanya Arsenal kufungwa kwa mara ya
kwanza mechi nne mfululizo za Ligi kwa mara ya kwanza chini ya Arsene Wenger.
Matokeo haya
yameiweka Arsenal nafasi ya 6 kwa pointi 54 sawa na Everton walio nafasi ya 7
wakiwa pointi sawa na Arsenal -54 huku Manchester
United wakishika nafasi ya 5 kwa pointi 57 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Timu ya 4
Man City lakini wao wamecheza Mechi 1 pungufu.
|
Mashabiki wengi wa Arsenal nao hawakubaki nyuma kumtaka Mzee Wenger wakimlalamikia aondoke katika
timu hiyo kutokana na kutopatia mataji kwa zaidi ya miaka kumi sasa.
|
Mechi nne
ilizofungwa mfululizo za ugenini Arsenal na Chelsea 3-1, Liverpool 3-1, West
Bromwich na Jana April 10, 2017 imepoteza 3-0 dhidi ya Crystal Palace lakini
hicho kinakuwa ni kipigo cha kwanza toka Arsenal ipate ushindi wa kwanza wa EPL
April 6 2017 dhidi ya West Ham United baada ya siku 53 bila kupata ushindi,
mfululizo wa matokeo hayo kuna hatarisha nafasi ya Arsenal kucheza Champions
League msimu ujao.
|
No comments:
Post a Comment