Simba SC imeilazimisha
Mbeya City sare ya kufungana magoli 2-2 katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara
uliochezwa leo March 4, 2017,kwenye uwanja wa taifa.
Mbeya City
walianza kupata goli la kuongoza kipindi cha kwanza lililofungwa na Ditram Nchimbi dakika ya 37 kipindi cha
kwanza baada ya kuachia shuti kali kufatia kupokea pasi ya kisigino ya Raphael
Daudi.
Ibrahim Ajib aliisawazishia Simba SC dakika ya 65
kipindi cha pili kwa mpira wa adhabu ndogo baada ya Mohamed Ibrahim kuangushwa nje kidogo ya box la penati. Ajibu aliuchinja mpiara na kuukwamisha
kwenye nyavu huku golikipa wa Mbeya City Owen
Chaima akiruka bila mafanikio.
Mbeya City
hawakukata tamaa, dakika 75 Kenny Ally
akaifungia Mbeya City bao la pili baada ya kugongeana pasi na Raphael Breyson ambaye alipiga pasi kwa
Ditram Nchimbi aliyepiga pasi ya
mwisho kwa Kenny Ally na kukwamisha
mpira kambani.
Dakika
zikiwa zimeyoyoma Simba SC wakapata goli la kusawazisha kwa mkwaju wa penati
kufatia beki wa kushoto wa timu hiyo, Mohamed
Hussein ‘Tshabalala’ kuangushwa kwenye box.
Mkwaju wa
penati ukapigwa na Shiza Ramadhani
Kichuya na kuamua game hiyo kumalizika kwa sare ya kufungana 2-2.
Sare ya leo
imeifanya Simba SC kuongeza pointi moja na kufikisha pointi 55 baada ya kucheza
mechi 24, ipo mbele kwa pointi tatu dhidi ya Yanga SC yenye pointi 52 lakini
inamchezo mmoja ambao itacheza kesho Jumapili February 4, 2017 dhidi ya Mtibwa
Sugar.
Simba SC ni
mara ya pili inapata matokeo ya sare ya kufungana 2-2 dhidi ya Mbeya City
kwenye uwanja wa taifa, mara ya mwisho kupata matokeo kama hayo ilikuwa ni
September 21, 2013.
|
No comments:
Post a Comment