Madaktari
nchini Kenya, wamefanikiwa kuishawishi mahakama nchini humo kuzuia kuajiriwa
kwa madaktari 500 kutoka Tanzania.
Madaktari
hao walienda mahakamani kuizuia serikali ya nchi hiyo kutoa ajira hizo wakidai
kuwa kuna madaktari 1,400 wasio na ajira nchini humo.
Wamelalamika kuwa itakuwa
ni ufujaji wa fedha kuwa na madakrari 500 wa Kitanzania watakaolipwa tshs
360,000 kwa siku. Mahakama ya kazi imetoa agizo hilo Ijumaa hii (March 31,2017),
ikisema kuwa litadumu hadi ombi la maofisa wa afya litakaposikilizwa na
kuchambuliwa.
“That leave
is hereby granted…to quash the decision of the government…to hire foreign
doctors to be deployed to Kenya,” zimesema nyaraka za mahakama za March 31.
Mahakama
hiyo imetoa siku 21 kwa serikali kuwajibu maofisa hao na suala hilo litatajwa
April 19.
Mwezi huu
Rais Dkt John Magufuli alisema kuwa Tanzania itapeleka madaktari 500
kukabiliana na uhaba uliopo na tangazo la nafasi hizo lilitolewa kuwataka wenye
sifa kutuma maombi.
Hata hivyo mpango huo umepingwa vikali na baadhi ya
viongozi wa nchini humo akiwemo Raila Odinga, ambaye ni rafiki wa karibu na
Rais Magufuli.
Chanzo: The Star Kenya
|
Friday, March 31, 2017
Mahakama ya Kenya yazuia kuajiriwa kwa madaktari 500 toka Tanzania.
Tags
# MATUKIO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MATUKIO
Labels:
MATUKIO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment