Mkurugenzi
wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa
Wakurugenzi Nchini.
|
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija (Kushoto) ambaye
kachaguliwa kuwa katibu wa Wakurugenzi nchini.
|
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg
John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA
wa Wakurugenzi Nchini.
Na
Mathias Canal, Dodoma.
Wakurugenzi
wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa kote nchini Tanzania, kwa kauli moja wameridhia na
kuwachagua Viongozi watakaowawakilisha katika kufikisha changamoto zao
mbalimbali katika ngazi za juu ili kupungunza uwasilishaji wa kila Mkurugenzi
kufikisha changamoto zake ngazi za juu.
Uchaguzi huo
umefanyika hii Leo katika ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma kwa maridhiano ya
Wakurugenzi wote kwa asilimia 100% ya kura zote.
Uchaguzi huo
umejiri Mara baada ya kumalizika kikao cha kazi kilichoongozwa na Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Eng Musa Iyombe
kilichohudhuriwa na Wakurugenzi wote 185.
Wakurugenzi
hao wamefanya uchaguzi kwa nafasi nne ambazo ni Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti
sambamba na Katibu Mkuu na Muweka Hazina.
Wakurugenzi
waliochaguliwa katika nafasi hizo ni-
1.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa
Mwenyekiti
2.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Ndg Rachel Chuwa ambaye kachaguliwa
kuwa Makamu Mwenyekiti.
3.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija, ambaye
kachaguliwa kuwa katibu.
Na
4.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti Mara baada ya uchaguzi huo kumalizika Viongozi hao
waliochaguliwa wameeleza namna bora ya kuhumiza uwajibikaji kwa Wakurugenzi
wote sambamba na kuwawakilisha vyema kufikisha changamoto zao kwa ngazi za juu.
Wameueleza
mtandao wa www.wazo-huru.blogspotm.com kuwa
imani kubwa waliyopatiwa na Wakurugenzi wote nchini ya kuwachagua kuwa
wawakilishi wao ni kubwa hivyo wana kila sababu ya kuitumikia kwa weledi na
usawa.
"Kupitia
Wawakilishi hao waliochaguliwa Wakurugenzi nchini wataraji utendaji uliotukuka
na uwakilishi unaostahili kulingana na changamoto zinazowakabili katika maeneo
yao" Alisema MD Kayombo John L.
|
No comments:
Post a Comment