Mkuu wa Mkoa
wa Ruyigi, Bw. Abdalah Hassan mwenye kofia Nchini Burundi na Mkuu wa Wilaya Kibondo mkoani Kigoma nchini Tanzania, Bw.Luis Bura
walipokuwa katika kikao cha ujirani Mwema
Nchini Burundi.
Kutokana na
hali ya usalama kwenye mipaka ya nchi za Burundi na Tanzania kulegalega kwa
kushamili vitendo vya uharifu wa kutumia siraha Kamati ya ulinzi na usalama
wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma nchini Tanzania imekutana na Kamati za ulinzi za mikoa ya Chankuzo,
Ruyigi, Kitega nchini Burundi na kuweka mikakati ya kuzuia uharifu huo
unaoendelea kugharimu maisha ya watu na mali zao.
Akiongea
katika Kikao hicho kilichofanyika March 27, 2017 Mkoani Ruyigi Nchini Burundi
mkuu wa wilaya ya Kibondo Tanzania,Bw.
Luis Bura alisema makundi ya uharifu yanayoonekana kuvuka mipaka na kufanya
ujambazi kwa kufanya mauwaji yanakuwa ni tishio kwakuwa Watanzania hivi sasa
hawafanyi kazi zao kwa amani na kuvitaka vyombo vya ulinzi pande zote
kushirikina.
|
‘’Makundi ya
waharifu wanao tumia siraha wanaonekana kuvuka mika na kuingia nchini mwetu
kuuwa watu sasa mauwaji ya raia wetu sasa basi kinachotakiwa kamati zenu na
serikali kwa ujumla kuliangalia kwa umakini mkubwa jambo hili maana ni hatari
sana watu wet kwa sasa hawafanyi kazi zao kwa amani kwa kuhofia kuvamiwa hata
mashambani hawaendi ''...alisema Bura.
Kwa upande
wake mkuu wa Mkoa wa Ruyigi Abdalah Hassan alisema ili kuwepo mafanikio
katika vita dhidi ya uharifu lazima vyombo husika pande wajenge utaratibu wa
kukutana kila mara ili kujadiri namna na kupeana taarifa za haraka
kushirikiana
Mkuu wa
upelelezi wa Mkosa ya Jinai wilayani Kibondo upande wa Tanzania, Rutatinisibwa
Tibyeilwa aliitaka Serikali ya Burundi kudhibiti uzagaaji wa siraha za Moto
kwakuwa watu wamekuwa wakikamtwa nchini Tanzania wanapohojiwa, udai kuwa wanazinunua
Burundi
|
Baadhi ya
wajumbe wa Kamati za ulinzi na usalama Wilayani Kibondo,Mkoani Kigoma nchini Tanzania na wenzao wa Mikoa ya Ruyigi Chankuzo na
Kitega nchini Burundi walipokuwa katika kikao cha ujirani mwema.
‘’ Siaraha
nyingi za Moto zimekuwa zikikamatwa katika maeneo mengi ya nchi yetu
mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Tabora, Mara, Dar Es Salaam na wahusika wanapohojiwa
ueleza kuwa wanazinunua huku kwenu nchini Burundi na zimekuwa zikisababisha
madhala makubwa sana hivyo tunaomba mjitahidi kudhibiti hali hiyo kwa kuwa si
nzuri''... alisema Rutatinisibwa.
Mkuu wa
usalama wa Jimbo la Ruyigi na Chankuzo, Kanal Elia Ndizigiye amekieleza kikao
hicho kuwa nchi ya Burundi ilipoingia katika matatizo wahasi walikimbia na
siraha nyingi zikiwemo sare za jeshi hivyo hao ndo chanzo cha uzagaaji wa
siraha bila utaratibu ili kudhibiti hali hiyo lazima ufanyike mkakati maalum.
HABARI/PICHA Na Muhingo Mwemezi-Kibondo/Kigoma.
|
No comments:
Post a Comment