Mkuu wa
Idara ya Habari na Mawasilianio wa Chadema, Tumaini Makene amesema leo (Alhamisi) kuwa chama hicho
kupitia Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe, baada ya kesi ya kikatiba
namba 1 ya mwaka 2017 inayotarajiwa kuwasilishwa Mahakama Kuu leo, kitazungumza
kwa umma kupitia waandishi wa habari kuwakaribisha wanachama wapya waliojiunga
leo akiwemo Wema Sepetu.
|
Wema pamoja
mama yake, leo aliongozana na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe pamoja na
viongozi wengine wa chama hicho kwenye mahakama kuu jijini Dar es Salaam.
Msanii huyo
aliyeshinda taji la Miss Tanzania mwaka 2006, alikuwa kada wa Chama cha
Mapinduzi (CCM) kabla ya kuhamia Chadema.
|
No comments:
Post a Comment