Pia Mhe.
Rais Magufuli amempongeza Mama Mariam Amir (Bibi Mwanja) kwa upendo wake wa
kumchukua Neema na kisha kumpa hifadhi nyumbani kwake huko Tandika Devis Kona
Jijini Dar es Salaam.
“Nakushukuru
sana Mama na ninakupongeza, umeonesha mfano mzuri wa kujali umoja na upendo kwa
Watanzania wenzako bila kujali dini, kabila wale kanda unayotoka na hivi ndivyo
Watanzania wote tunapaswa kufanya” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Kabla ya
kutoa pongezi hizo, mapema leo asubuhi Mhe. Rais Magufuli amewatuma wasaidizi
wake wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Gerson Msigwa
kwenda Tandika Devis Kona katika Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam kumuona
Neema Mwita Wambura ambaye alipatiwa hifadhi katika nyumba ya Mama Mjane
aitwaye Mariam Amir (Bibi Mwanja) baada ya kuona picha na kusoma taarifa za
mkasa uliomkuta katika mitandao ya kijamii.
Mhe. Rais
Magufuli ametoa Shilingi laki 5 kwa Neema kwa ajili ya kumsaidia chakula yeye
na watoto wake waliohifadhiwa na rafiki yake huko Bunda Mkoani Mara na pia
ametoa Shilingi laki 5 kwa Mariam Amir aliyejitolea kumsaidia na kumpa hifadhi
nyumbani kwake.
Pia ameahidi kumsaidia wakati wote wa matibabu na pia familia
yake.
|
Baada ya
kumpokea daktari bingwa wa magonjwa ya dharula na ajali katika kitengo cha
dharula cha Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga amesema wameanza
kumfanyia uchunguzi ili kujua maendeleo yake na kama kumpa matibabu zaidi.
Nae Daktari
Bingwa wa Upasuaji Dkt. Ibrahim Mkoma ambaye amekuwa akimfanyia matibabu Neema
Mwita Wambura tangu Julai 2015 alipofikishwa hospitalini hapo kwa mara ya
kwanza amesema Neema anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji mara nne.
Dkt. Mkoma
amesema baada ya upasuaji huo, sasa Neema anaweza kuinua na kugeuza shingo yake
na kwamba kwa sasa wataendelea kumfanyia uchunguzi zaidi ili kujua maendeleo
yake.
Mhe. Rais Magufuli ameagiza vyombo vyote vinavyohusika kufanyia kazi
mkasa uliomkuta Neema Mwita Wambura na kuhakikisha haki inatendeka.
|
No comments:
Post a Comment