Toka ukiwa
mdogo mpaka unazeeka umekuwa ukijiuliza kwanini kila kitu unachokula au
kukionja huwa kinakuwa na ladha mbaya mara tu baada ya kusafisha kinywa chako
kwa kutumia mswaki ulioweka dawa ya meno.
Dawa nyingi
za mswaki huwa zinakemikali zifuatazo Sodium lauryl sulfate, sodium laureth
sulfate (SLS) and sodium lauryl ether sulfate (SLES) ambazo hupunguza nguvu ya
ukinzani ili kutengeneza povu (foaming action) kwenye dawa ya meno ili kusaidia
katika kuondoa mabaki ya vyakula kwenye kinywa chako.
Lakini pia
kemikali hizi hukinzana na utendaji kazi wa taste buds (huhusika na utambuzi wa
ladha) kwa kuvunja vunja phospholipids kwenye ulimi wako.
Matokeo yake
husababisha ladha ya uchachu (bitter tastes) nahii ndo sababu kila unachokionja
na kukila huonekana kibaya mara baada ya kusafisha meno yako.
Lakini hali
hii huondoka mara tu baada ya mda mfupi. Niwatoe hofu watumiaji wa dawa za meno
kuwa hali hii ya kuhisi uchachu haina madhara yeyote kiafya.
Your Health,
Our Concern
Imeandaliwa
na;
FORD A.
CHISANZA
Scientist/Researcher/pharmacist
Location:
Off Mandela Road, Mabibo – External,
P.o.Box:
77150, Dar Es Salaam, Tanzania.
Mobile:+255
652466430/+255 684363584
Email:
fordchisanza@gmail.com
|
No comments:
Post a Comment