VPL 2016/2017 :- Simba SC yapunguzwa kasi na Mitbwa Sugar -Jamhuri, Morogoro. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, January 18, 2017

VPL 2016/2017 :- Simba SC yapunguzwa kasi na Mitbwa Sugar -Jamhuri, Morogoro.

Simba SC wamebanwa mbavu katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Leo hii January 18,2017 baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji, Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

 Matokeo hayo yanayoiongezea kila timu pointi moja na yanaifanya Simba SC ifikishe pointi 45 baada ya kucheza mechi 19 na sasa wanawazidi kwa pointi mbili tu, mabingwa watetezi, Yanga SC.

Hapo Jana,January 17, 2017 Yanga SC, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa VPL, walicheza Ugenini huko Uwanja wa Majimaji Jijini Sokoine na kutoka na ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya Majimaji FC kwa Bao la mapema la Deus Kaseke .

Usiku huu, huko Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, Azam FC watacheza na Mbeya City katika Mechi ya VPL.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad