UTANGULIZI.
Kufuatia
ongezeko wa matukio ya ajali za barabarani mkoani Kagera, Radio FADECO imeamua
kushiriki, kuwashirikisha na kuunga mkono jitihada zinazofanywa kutokomeza
ajali za barabarani kwa kuwaalika wadau wote wa usalama barabarani mkoani
Kagera na pengineko, kuungana katika kampeini ya ZUIA AJALI HAPA kwa kutoa
elimu ya usalama barabarani kupitia SHULE ZOTE ZA MSINGI, SEKONDARI na VYUO VYA
ELIMU YA JUU NA UFUNDI mkoani Kagera.
Pamoja na kuendesha na kuruhusu vipindi
vya usalama barabani redioni mara moja kwa wiki, sasa RADIO FADECO kwa Kushirikiana na Radio nyingine za Mkoani Kagera kuendeleza kampeini hii mashuleni.
KWA NINI
KUELEKEZA MKAKATI WA ELIMU YA USALAMA BARABARANI MASHULENI (SHULE ZA MSINGI,
SEKONDARI, VYUO VYA ELIMU YA UFUNDI NA YA JUU)?
Wanafunzi
kama WAHANGA WAKUU NA WALENGWA MAHUSUSI:
Wanafunzi
kama sehemu ya watumia barabara na walengwa wakuu wa usalama barabarani, hawana
budi kuelimishwa juu ya usalama barabarani,
·
kwani
kila siku wanatumia barabara wanapokwenda shule au wanaporudi kutoka
shuleni.
·
Kwa
kuwa wanatumia barabara kila siku, hawana budi kuzifahamu na kuzifuata sheria
za usalama barabarani.
·
Wao pia kama abiria wakiwa wakisafiri,
wanakuwa na jukumu la kusaidia katika kuelimisha, kukumbushia na kufuatilia
matumizi ya sheria na kanuni za usalama barabarani.
·
Lakini wao pia kama madreva wa kesho, ni vema
waanze harakati za kupata leseni za udreva wakiwa tayari wanazijua sheria na
kanuni za usalama barabarani (si kama inavyokuwa siku hizi katika vyuo vya
udereva, kuanza kufundisha alama za usalama barabarani, n.k.)
KAMA
WAKUFUNZI WA WENZAO NA JAMII KWA UJUMLA HUSUSANI WAZAZI WAO (PEER
EDUCATORS)
Wanafunzi
wanakuwa WAKUFUNZI wazuri kwa wazazi na ndugu zao wa karibu, na kwa wananchi
wote kwa ujumla, hivyo tukipandikiza mbegu ya kutii sharia za usalama
barabarani kwao, tunakuwa tumepandika mbegu ya kudumu.
SHULE
ZINATOA FURSA YA MIKUSANYIKO MIKUBWA KWA WAKATI MOJA KILA SIKU (SCHOOLS PROVIDE
OPPORTUNITY FOR MASS GATHERING IDEAL FOR MASS SENSITIZATION CAMPAIGNS)
Shule zote
ziwe za msingi, sekondari au vyuo, zina mkusanyiko na idadi kubwa wa watu kwa
kila wakati.
Zipo shule zenye wanafunzi kuanzia 100 huku zingine zina wanafunzi
zaidi ya 500.
Mkusanyiko huu unaopatikana kwa wakati moja na kila siku, ni
fursa kubwa ya kutoa hamasa na elimu ya usalama barabarani.
MPANGO WA
RADIO FADECO NA WADAU (PROPOSED PLAN OF FADECO RADIO WITH PARTNERS):
1.
Kushirikiana na wadau wote wa usalama barabarani na wa maendeleo na wananchi
wote kwa ujumla katika kampeini hii ya ZUIA AJALI HAPA. Wadau hawa ni pamoja na
JESHI LA POLICE, VYUO VYA UDEREVA, WAHISANI NA WANANCHI WOTE KWA UJUMLA.
2.
Kutengeneza na kusambaza vibao na vipeperushi vya alama za usalama barabani
kuanzia kila shule ya msingi, sekondari na vyuo.
Na baadae katika kila ofisi ya
serikali na sehemu yeyote yenye mkusanyiko mfano dispensary, hospitali, ofisi
za serikali na taasisi.
3. Kuomba Idara ya elimu ya mkoa na wilaya pamoja na
uongozi wa shule, kuruhusu kuanzisha KIRANJA wa usalama barabarani katika kila
shule. KIRANGA HUYU atakuwa kama AFISA USALAMA BARABARANI katika kila shule.
Atafundishwa Zaidi kusimamia usalama wa wanafunzi wenzake katika shule husika. Atapewa
vazi rasmi la usalama barabarani la kumutambulisha na ataombwa kulivaa kila
siku anapokuwa shuleni au akitoka nyumbani kuja shule.
4. Kuendesha vipindi vya
usalama barabarani redioni kila wakati 5. Kuomba ushiriki wa RADIO ZOTE za mkoa
wa kagera (RADIO KWIZERA, FADECO, KASIBANTE, KARAGWE na RADIO VISION) kushiriki
katika kampeini hii.
Kuendesha mafunzo kwa waandishi wa habari na watangazaji
jinsi ya kutoa taarifa na elimu juu ya usalama barabarani.
6. Kusaidiana na
wadau wa usalama barabarani katika kuhakikisha kuwa, tunaanzisha mitandao ya
ROAD SAFETY AMBASSADORS katika ngazi ya kila wilaya.
7. Kuanzisha utaratibu wa
kupashana taarifa za usalama barabarani kwa njia ya Radio au TEHAMA.
Walengwa: Shule za Msingi 925 Shile za sekondari 345 Vyuo vya elimu ya juu 37
WADAU KATIKA
KAMPENI HII.
RADIO ZA
JAMII NA ZINGINE MKOANI KAGERA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI, JESHI LA POLISI
KAGERA KAMATI ZA USALAMA BARABARANI ZA WILAYA ZOTE KAGERA VYUO VYA MAFUNZO YA
UDEREZA IDARA YA ELIMU NA SHULE ZOTE MKOANI KAGERA
|
No comments:
Post a Comment