Uzalishaji
katika kiwanda cha saruji cha Dangote kilichopo Mtwara umesimama kwa muda
kutokana na hitilafu za kiufundi zilizojitokeza katika mitambo.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Dangote Tanzania, Harpreet Duggal alisema jana kwamba mafundi
wa Dangote wapo kazini na shughuli za uzalishaji zitarejea katika siku chache
zijazo.
Alisema
kiwanda kinachomilikiwa na bilionea namba moja Afrika, Alhaji Aliko Dangote wa
Nigeria kilianza uzalishaji wa kibiashara mwaka huu na kama ilivyo kwa kiwanda
kingine kama hicho, jambo lolote linaweza kutarajiwa hasa katika miezi ya
mwanzo.
Alisisitiza,
“hitilafu hizi ni za kawaida na uzalishaji utarejea katika kipindi kifupi kijacho.”
Akizungumzia
gharama za uzalishaji, Duggal alisema uendeshaji nchini uko juu huku miongoni
mwa sababu ikiwa ni matumizi ya jenereta za dizeli katika kuendesha kiwanda.
Hata hivyo,
alisema serikali inaangalia suala hili la gharama na jinsi ya kutafuta njia ya
kuwapunguzia mzigo.
|
No comments:
Post a Comment